Papa Leo wa 1XIV anajiandaa kusafiri hadi Lebanon baadaye mwaka huu, ambayo inaweza kuwa safari yake ya kwanza nje ya nchi tangu kuchaguliwa kuwa mkuu wa Kanisa Katoliki mwezi Mei.
Askofu Mkuu Paul Sayah, naibu wa kiongozi wa ngazi ya juu kabisa wa Kanisa Katoliki nchini Lebanon, aliiambia BBC kuwa Vatican "inatathmini" safari hiyo lakini kanisa bado linasubiri tarehe rasmi.
Ziara hiyo itaashiria wakati muhimu kwa Papa wa kwanza wa Marekani, ambaye amesisitiza mara kwa mara amani katika Mashariki ya Kati na kuwepo kwa madhehebu mbalimbali.
"Lebanon ni nchi yenye tamaduni nyingi, yenye dini nyingi na ni mahali pa mazungumzo," Askofu Sayah alisema.
"Ni moja ya mazingira adimu ambapo Waislamu na Wakristo wanaishi pamoja na kuheshimiana... hivyo inatuma ujumbe kwa ukanda huo."
Kumekuwa na tetesi kuhusu ziara ya kwanza ya Papa ambayo huashiria msimamo wake.
Safari kuu ya kwanza ya Baba Mtakatifu Francisko nje ya Roma, hadi kisiwa cha Lampedusa nchini Italia mwaka 2013, iliweka mazingira ya kuzingatia kwa suala la uhamiaji na jamii zilizotengwa.
Katika miongo ya hivi karibuni, safari za nje zimekuwa zikizingatiwa na papa, na hivyo kuwaruhusu mapapa kuungana na Wakatoliki duniani kote, kueneza ujumbe wao na kushiriki katika diplomasia.
Katika miaka yake 12 kama papa, Francis alitembelea nchi 68 katika safari 47 za nje, mara nyingi akichagua maeneo yenye jamii masikini, ambayo alielezea kama "sehemu muhimu " za Kanisa.
Lebanon, maoa ya zaidi ya Wakatoliki milioni mbili na inayojulikana kwa utofauti wake wa kidini, kwa muda mrefu imekuwa na uzito wa mfano kwa Kanisa. Kufika huko kwa papa huko pia kunnaweza kumuweka Leo karibu na vita huko Gaza na mzozo mkubwa wa Israeli na Palestina.
"Kila mtu anazungumza na Israel lakini Israel haisikii. Netanyahu haonekani kusikiliza sana, lakini kadiri [viongozi wanavyozungumza] ndivyo inavyokuwa bora," Askofu Sayah alisema.
"Ikiwa Papa ataongeza sauti yake na wasiwasi, nadhani kuna uwezekano wa kuwa na athari fulani."
Papa Leo tayari ametoa tahadhari kwa juhudi za kuwafikia watu na imani nyingine.
Moja ya mikutano yake ya kwanza baada ya kuchaguliwa kwake ilikuwa na wajumbe wa dini mbalimbali, ambapo alisifu "mizizi ya Kiyahudi ya Ukristo" na kuheshimu "kujitolea kwa mazungumzo na udugu" kati ya Wakatoliki na Waislamu. Amesisitiza mara kwa mara Wakristo, Wayahudi, na Waislamu "kusema hapana kwa vita na ndio kwa amani".