Marekani na Venezuela kurejesha uhusiano wa kidiplomasia baada ya Maduro kukamatwa

Chanzo cha picha, Getty Images
Marekani na Venezuela zimekubaliana kurejelea tena uhusiano wa kidiplomasia na kibalozi.
Taarifa zinasema pande hizo mbili zitafanya juhudi za pamoja ili kukuza utulivu, kuunga mkono ufufuaji wa uchumi na kuendeleza maridhiano ya kisiasa.
Wakati uhusiano wao wa kidiplomasia umekuwa ukiimarika tangu jeshi la Marekani lilipomkamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro mwezi Januari katika shambulio la kushtukiza, kutangazwa kwa uhusiano rasmi wa nchi hizo mbili kunaashiria hatua kubwa.
Rais Donald Trump aliamuru wanajeshi kumkamata Maduro na mkewe, na kuwafikisha katika mahakama ya Manhattan kujibu mashtaka ya kutumia silaha na dawa za kulevya, madai ambayo wanayakanusha.
Soma pia:




