Walaghai wa Kichina wafukuzwa nchini Nigeria

Chanzo cha picha, Economic and Financial Crimes Commission/X
Nigeria imewafukuza raia wa kigeni, wakiwemo raia 50 wa China, katika msako mkali uliofanyika wiki iliyopita dhidi ya mojawapo ya "makundi makubwa zaidi ya uhalifu wa mtandaoni yanayoongozwa na wageni", wakala wa kupambana na ufisadi nchini humo umesema.
"Hii inaleta jumla ya raia wa kigeni waliotiwa hatiani kufikia 102 katika zoezi linaloendelea," ilisema, na kuongeza kuwa wamepatikana na hatia ya "ugaidi wa mtandao na udanganyifu wa mtandao".
Ni miongoni mwa wageni 192 waliokamatwa wakati wa operesheni kali huko Lagos Ijumaa iliyopita.
Nigeria inajulikana kwa ulaghai kwenye mtandao na ulaghai wa mapenzi.
Kesi za uhalifu wa mtandaoni zilikuwa miongoni mwa makosa yaliyoenea zaidi nchini Nigeria mwaka jana, kulingana na Tume ya Uhalifu wa Kiuchumi na Kifedha (EFCC).
Katika miaka ya hivi majuzi, EFCC imefanikiwa kuteka maficho kadhaa ambapo vijana wahalifu mtandaoni, wanaojulikana kama "Yahoo Boys", hujifunza ujuzi wao wa kulaghai.
Pia kumekuwa na kesi kadhaa za juu za ulaghai wa mtandaoni zinazohusishwa na Wanigeria wanaoishi nje ya nchi, baadhi zilifichuliwa na Ofisi ya Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI).
Mwaka jana, mmiliki wa Instagram, Meta, aliondoa maelfu ya akaunti nchini Nigeria ambazo zilikuwa zikijaribu kulenga watu katika miradi ya ulaghai mtandaoni.
Walaghai kama hao kwa kawaida hujifanya kama wanawake mtandaoni ili kuwalaghai watu kutuma nyenzo chafu za ngono kabla ya kuwachafua.
Kampuni hiyo ilisema pia iliondoa vikundi 5,700 vya Facebook ambapo walaghai walikuwa wakitoa vidokezo kuhusu jinsi ya kuwalaghai watu.
Wataalamu na mamlaka hapo awali waliwaonya watumiaji wa mitandao ya kijamii kuendelea kufahamu na kuwa macho kuhusu hatari za ulaghai huo.
Unaweza kusoma;













