Kujifunza lugha mpya: Je ni umri gani unaweza kujifunza?

Girls during a Belarusian language lesson at a secondary school in the village of Osinovka

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Masomo ya lugha ya Belarusi: Vijana wanafaida zaidi ya watoto wadogo na watoto wachanga inapokuja katika suala ya kujifunza lugha mpya

Ni wakati wa majira ya kipupwe asubuhi katika shule ya chekechea ya mafunzo ya Lugha ya Kihispania mjini London.

Wazazi wanawasaidia watoto wao wadogo kuvaa kofia ngumu ili kuwakinga na ajali za baiskeli wanazoziendesha. Waalimu wanawasalimia watoto kwa maneno "Buenos días!"

Miongoni mwa watoto waliokuwa wakicheza kwenye umwanja wa shule, kasichana kadogo kanaomba kasaidiwe kusaidiwe kufunga nywele zake nyuma mtindo unaoitwa "coleta" kwa lugha ya Kihispania. Na baadae kakapiga mpira huku kakipaza sauti na kusema "Catch!" ikimaanisha ''kamata!'' kwa lugha ya kiingereza.

"Katika umri huu, watoto hawajifunzi lugha-wanaipata lugha ," anasema mkurugenzi wa shule Carmen Rampersad.

Kwa baadhi yao inaonekana hawatumii juhudi zozote kujifunza.

Children in a classroom, sitting on the carpet clapping hands

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Watoto wadogo hujifunza haraka lafudhi za lugha zao za asili -lakini faida za ujuzi wa lugha huja kadri mtu anavyoendele kukua.

Wengi miongoni mwa watoto , Kihispani ni lugha yao ya tatu au hata ya nne . Lugha mama ni pamoja na Kicroatia , Kiebrania, Kikorea na Kiholanzi.

Ukilinganisha kujifunza kwao na jinsi mtu mzima mwenye umri wa wastani anavyohangaika katika darasa la lugha , inaweza kuwa rahisi kusema kuwa ni bora kuanza kujifunza lugha ukiwa mtoto.

Lakini sayansi inatoa mtizamo mgumu zaidi kuhusu jinsi mahusiano yetu na lugha yanavyobadilika na kukua katika kipindi chote cha maisha yetu- na kuna sababu nyingi za kuwatia moyo wanaojifunza lugha baadae maishani mwao.

Kwa ujumla, hatua tofauti za maisha yetuhutrupatia faida tofauti katika kujifunza lugha.

Tuwapo watoto wachanga , tunakua na sikio linaloweza kutambua aina tofauti za sauti, tunapokua watoto wadogo tunaweza kutambua haraka lafudhi zetu za asili kwa kasi kubwa ya kushangaza.

Kama watu wazima, huwa tunakua na uwezo wa kumakinika na matamshi ya lugha na vilevile tunakua na ujuzi muhimu wa mambo mbalimbali, kama kujua kusoma na kuandika, ambao hutuwezesha kupanua wakati wote matamshi yetu, hata katika lugha zetu wenyewe.

Na utajiri wa mambo zaidi ya utu uzima - kama hali za jamii, njia za kufundishia, na hata upendo na urafiki- vinaweza kuchangia idadi ya lugha tunazoweza kuzizungumza na ubora wake.

Kutumia sehemu kubwa ya ubongo wako

An older woman, wearing a sari, taking notes - close up of her hands and note pad

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Adults were better at grasping arbitrary language rules

"Sio kila kitu kina kinazeeka kutokana na umri wetu ," anasema Antonella Sorace,profesa wa maendeleo ya lugha na mkurugenzi wa kituo masuala ya lugha -Bilingualism Matters Centre katika Chuo Kikuu cha Edinburgh.

Anatoa mfano wa kile kinachofahamika kama ' explicit learning': ikimaanisha kujifunza lugha darasani pamoja na mwalimu anayeelezea kanuni za lugha.

" Watoto wadogo hufanya vibaya sana katika explicit learning, kwasabu hawana udhibiti wa utambuzi na umakini pamoja na uwezo wa kukumbuka ," Sorace anasema.

Utafifi ulioendeshwa na Israeli, kwaulibaini kuwa watu wazima walikua bora zaidi katika kung'amua kanuni za lugha bandia fna kuzitumia katika hali halisi wawapo kwenye maabara.

Wanasayansi walilinganisha makundi tofauti matatu : wenye umri wa miaka mika 8, miaka 12 na vijana . Watu wazima walipata alama za juu kuliko makundi yote mawili ya watoto wadogo , na wale wamiaka 12 walifanya vema kuliko watoto wadogo sana.

A group of young students, walking in campus

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Baadhi ya watafiti wamebaini kuwa vijana wadogo wana taarifa nzuri juu ya dunia zinazowasaidi katka kuelewa dhana mpya

Hii imetokana na utafiti wa muda mrefu uliofanywa kwa wanafunzi 2,000 waliokuwa wakijifunza lugha mbili za Kicatalonia- Kihipania ambao walikua wanazungumza Kiingereza : Walianza kusoma lugha hizo wakiwa watu wazima walielewa haraka kuliko vijana wadogo waliokua wanajifunza kwa mara ya kwanza.

Nguvu ya ubongo wa kijana mdogo

Watafiti nchini Israeli wanasema kwamba mshiriki wao ambaye alikua mtu mzima huenda alifaidika kutokana na ujuzi unaokuja na utu uzima - kama vile mikakati ya kutatua tatizo- na ujuzi wa muda mrefu wa lugha.

Kwa maneno mengine, wanafunzi wakubwa kwa umri huwa tayari wanajuam mambo mengi kuwahusu na dunia na wanaweza kutumia ujuzi juu kutambua taarifa mpya.

Watoto wadogo ni bora zaidi kujifunza wakiwa pamoja na mwalimu ana kwa ana: Kusikiliza mzungumzaji wa lugha asilia na kuiga uzungumzaji wake. Lakini aina hii ya kujifunza huhitaji muda mwingi wa kuwa pamoja na mzungumzaji asili wa lugha.

Kujifunza rahisi

Kwa kawaida sote huanza maisha yetu kama wataalamu wa lugha asili. Tukiwa watoto wachangatunaweza kusikia maneno na misemo 600 na herufi 200 yanayounda lugha duniani.

A baby crying

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Hata mtoto mchanga anapozaliwa hulia kwa lafudhi, kuiga maneno waliyosikia wakiwa tumboni

Katika kipindi cha mwaka wa kwanza wa maisha yetu, ubongo wetu, hunasa sauti tunazozisikia zaidi mara kwa mara.

Watoto wdogo mara nyingi huzungumza maneno kadhaa ya lugha za mama zao. Hata watoto wanapozaliwa hulia kwa lafudhi za sauti walizozisikia ndani ya tumba za mama zao.

Hii ina maanisha kuwa utambuzi wa lafudhi na maneno hayo hutusaidia kupunguza ujuzi wa yale tusiyoyahitaji : Watoto wa Kijapan wanaweza kutofautisha kati ya sauti za herufi 'l' na 'r' - lakini Wajapani watu wazima wanapata ugumu kuzitofautisha .

A mother and daughter playing with a ball on the street

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wakati familia inapohama kutoka nchi moja kuelekea nchi nyingine, mara nyingi watoto hujifunza lugha haraka- lakini hilo hutokana labda na kwamba wanahitaji kufanya hivyo

Tunahitaji kuwa na msukumo wa kujifunza ...

Trenkic anatoa mfano wa familia inayohamia katika nchi mpya ya kigeni.

Kwa kawaida , watoto hujifunza lugha haraka zaidi kuliko wazazi wao.

Watoto huhisi haja ya dharura ya kufahamu lugha ili kuweza kuchangamana na jamii wanaoyoipata : kuwa na marafiki, kukubalika na kuchangamana na jamii.

Katika utafiA 2013 study of British adults in an Italian beginners' course found that those who stuck with it were helped by bonding with the other students and the teacher.

Mchakato mrefu wa maisha

mapema mwaka huu , utafiti uliofanywa uliofanyw kutokana na taasisi ya MIT ya huduma za mtandaoni kwa watu 670,000 ulibaini kuwa kufanikiwa kupata ujuzi wa sarufi ya lugha ya Kiingereza , ni vema kuanza kujifunza ukiwa na umri wa miaka 10 , baada ya hapo uwezo wa kujifunza hupungua.

A woman looking at the Thames river in London, UK

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Hata wazungumzaji wa lugha ya wazawa hujifunza walau neno moja kwa siku katika lugha yao hadi ewanapofikia umri wa kati

Hata hivyo utafiri unaonyesha kuwa, tunaweza kufahamu vyema lugha, ikiwemo lugha yetu asilia, baada ya muda.

Kwa mfano, tunaelewa sarufi kamili ya lugha zetu tunapotimiza miaka ipatayo 30.

Hii inaunga mkono, utafiti wa awali uliofanywa kwenye mtandao a,mbao unaonyesha kuwa hata wazungumzaji wa lugha yao asilia hujifunza takriban neno moja la lugha yao kila siku hati wanapotimiza umri wa kati wa maisha yao.

Kwanini tujijfunze lugha?

"Watu wakati mwingine huuliza, ni ipi faida kubwa ya kujifunza lugha ya kigeni?'' husema. " Kwani itanisaidia kupata pesa zaidi? Nitapata akili zaidi? Nitakua mwenye afya zaidi ?"

Close up of hands - older person using traditional tools of ink and brush to write Asian calligraphy

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Bado haujachelewa kujifunza lugha

"Lakini ukweli ni kwamba, faida kubwa ya kufahamu lugha za kigeni ni kuwa na uwezo wa kuwasiliana na watu zaidi ,"anasema

Trenkic ana asili ya Serbia. Aliweza kuzungumza Kiingereza bila matatizo alipokua na umri wa miaka 20 hivi tu, baada ya kuhamia Uingereza

Anasema bado anafanya makosa ya kisarufi , hususan wakati anapojaribu kusisitizia jambu fulani.