Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rebecca Kadaga ,Spika wa bunge la Uganda ataka waliomtesa Bobi Wine kukamatwa
Spika wa bunge la Uganda Rebecca Kadaga ametaka kukamatwa mara moja kwa polisi waliohusika kumpiga na kumjeruhi vibaya mbunge na mwanamuziki Bobi Wine pamoja na wabunge wenzake.
Kadaga ameandika barua hiyo kwenda kwa Rais wa Uganda Yoweri Museveni.
Bobi Wine ambaye jina lake kamili ni Robert Kyagulanyi, aliachiliwa kwa dhamana siku ya Jumatatu lakini akiwa katika afya dhoofu pamoja na makovu ya kipigo.
Mwanasiasa mwingine ambaye aliwekwa kizuizini pamoja naye Kassiano Wadri ameiambia BBC kuwa Bobi Wine alipigwa mara kwa mara na walinzi wa Rais ambao wengine walikua wamefisha nyuso zao.
Serikali imekanusha tuhuma hizo na kuziita za uongo.
Zaidi ya watu 30 walikamatwa wakihusishwa na uvamizi wa msafara wa Rais Museveni wiki mbili zilizopita na wote wameachiliwa kwa dhamana.