Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Urusi yazungumzia maandamano ya Jumapili na kuyataja kuwa uchokozi
Urusi imezungumzia maandamano makubwa yaliyoshuhudiwa siku ya Jumapili kwa kuulaumu upinzani kwa kuvunja sheria na kusababisha ghasia .
Vijana walilipwa kushiriki maandamano hayo kwa mujibu wa msemaji wa rais , lakini ameongeza kuwa ujumbe kutoka kwa maandamano yanayoambatana na sheria utasikilizwa.
Kiongozi wa upinzani nchini Urusi Alexei Navalny, ambaye ni mmoja wa mamia ya watu waliokamatwa alifikishwa mahakamani leo.
Alirejelea shutuma za ufisadi dhidi ya waziri mkuu Dmitry Medvedev.
Madai hayo ndiyo yalisabababisha maandamano ya siku ya Jumapili yaliyowafutia maelfu ya watu kote nchini humo ikiwemo miji ya Saint Petersburg, Vladivostok, Novosibirsk, Tomsk na miji mingine ukiwemo mji mkuu Moscow. Takriban watu 500 walikamatwa.
Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov, kwenye matamshi ya kwanza kutoka kwa urais, alisema kile walichokiona jana maeneo tofauti hasa mjini Moscow ni uchokozi na uongo.
Alisema kuwa kuwa vijana waliokuwa wameahidiwa kulipwa ikiwa wangekamatwa na polisi.
Bwana Peskov alipongeza hatua ya vikosi vya ulinzi na kutupilia mbali wito kutoka kwa Muungano wa Ulaya wa kutaka wale waliokamatwa kuachiliwa bila kuchelewa.
Alipoulizwa na BBC ikiwa bwana Medvedev atajibu madai ya ufisadi yanayomuandama, yaliyosababisha maelfu ya watu kuingia barabarani, bwana Peskov hakujibu lolote.