Anthony Joshua na Tyson Fury rasmi kuzichapa mwezi Disemba

Chanzo cha picha, Getty Images
Anthony Joshua amekubali masharti ya bingwa wa WBC Tyson Fury kwa ajili ya pambano la uzito wa juu linalowakutanisha waingereza litakalopigwa Disemba 3 mwaka huu.
Kampuni inayomsimamia bondia huyo, 258MGT inasema kwa sasa "anasubiri majibu", rasmi.
Joshua, 32, alipewa ofa na Team Fury, ambaye alipendekeza pambao liwe tarehe 3, disemba na mgao wa asilimia 60-40, bingwa Fury akipata asilimia 60.
Makubaliano ya Pambano yalifikiwa siku ya Ijumaa lakini tangazo lilicheleweshwa kutolewa kwa sababu ya kifo cha Malkia Alhamisi iliyopita.
Masharti ya awali yamekubaliwa lakini Joshua bado hajasaini mkataba. Katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wa Twitter ilisema: "258 na Matchroom Boxing wanaweza kuthibitisha, kwa niaba ya Anthony Joshua, kwamba tumekubaliana na masharti yote yaliyowasilishwa kwetu na timu ya Fury kwa ajili ya pambano hilo."
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Fury, 34, alisema angestaafu baada ya kumpiga Dillian Whyte mwezi wa Aprili, na akarudia madai hayo mwezi uliopita, kabla ya kumpa 'challenji' bingwa wa zamani wa dunia Joshua kupitia video iliyowekwa kwenye mtandao wa kijamii.
Joshua alipigwa na Oleksandr Usyk wa Ukraine katika mechi yao ya marudiano nchini Saudi Arabia mwezi uliopita, kikiwa ni kipigo chake cha tatu katika mapambano yake matano iliyopita.
Kuna kipengele cha mechi ya marudiano chenye mgawanyiko wa mapato ya nusu kwa nusu (50-50) ikiwa Joshua atamchapa Fury, lakini uukumbi utakaochapiwa pambano hilo la Desemba, bado haujathibitishwa.
Uwanja wa timu ya Cardiff, Principality Stadium unapigiwa chapuo, huku Saudi Arabia au nchi nyingine ya Mashariki ya Kati pia inaweza kuwa mwenyeji wa pambano hilo.















