Mossad: Operesheni za mafanikio na zilizoshindwa za shirika la kijasusi la Israel

Images of a bullet-ridden car, damaged buildings and an exploded pager sit on top of an Israeli flag

Chanzo cha picha, EPA, Getty, Maxar, BBC

    • Author, BBC News Arabic
  • Muda wa kusoma: Dakika 9

Wakati Israel iliposhambulia vituo vya nyuklia vya Iran, kambi za kijeshi na makazi ya watu binafsi, hasa magharibi mwa nchi hiyo na karibu na mji mkuu Tehran- mwezi Juni mashambulizi hayo yakitokea angani, iilishukiwa kuwa shirika la ujasusi la Israel, Mossad, pia lilihusika katika kuwatafuta walengwa na kutelekeza operesheni kutoka ardhini.

Mawakala wa Mossad wanaaminika kutumia ndege zisizo na rubani zilizoingizwa Iran kinyemela kulenga mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran, na Iran ilikiri kwamba inashuku kuwa maafisa wa ujasusi wa Israel wameingia Iran.

Idadi kubwa ya wakuu wa jeshi na wanasayansi wa nyuklia walilengwa tangu mashambulio ya Israel kuanza tarehe 13 Juni.

Hizi ni baadhi ya operesheni za mafanikio za Mossad:

Pia unaweza kusoma
Kuuawa Ismail Haniyeh
Ismail Haniyeh greeting IRGC commander Hossein Salami

Chanzo cha picha, Anadolu via Getty

Maelezo ya picha, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas Ismail Haniyeh (kushoto) akisalimiana na Kamanda wa Jesi la Mapinduzi ya Iran Hossein Salami (Kulia) alipotembelea Tehran - wote wawili wameuawa katika mashambulizi ya Israel.

Kiongozi wa kisiasa wa Hamas, Ismail Haniyeh aliuawa kwenye nyumba ya wageni jijini Tehran tarehe 31 Julai 2024. Miezi kadhaa baadaye waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz alikiri kuwa Israel ndiyo iliyohusika na mauaji hayo.

Khalil al-Hayya, afisa wa ngazi ya juu wa Hamas, aliuambia waandishi wa habari kwamba kombora lilimpiga Haniyeh "moja kwa moja,'' akinukuu mashahidi waliokuwa pamoja naye.

Lakini ripoti ya gazeti la New York Times, ambayo inawanukuu maafisa saba, ilisema Haniyeh aliuawa kwa bomu ambalo liliwekwa miezi miwili kabla katika jengo hilo.

BBC haiwezi kuthibitisha lolote kati ya madai haya.

Haniyeh ni mmoja wa viongozi wengi wa Hamas waliouawa na Israel tangu mashambulizi ya kundi hilo kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba 2023, akiwemo kiongozi wa Hamas huko Gaza, Yahya Sinwar, kaka yake Mohammed, mkuu wa tawi la kijeshi la Hamas, Mohammed Deif, na makamu wake, Marwan Issa.

Vifaa vya Hezbollah

Hezbollah fighters carry the coffin of Hussein Amhaz in front of crowds

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mazishi ya mpiganaji wa Hezbollah yanafanyika baada ya kuuawa na kifaa cha mawasiliano kilicholipuka
Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Tarehe 17 Septemba 2024, maelfu ya vifaa vya mawasiliano vililipuka kwa wakati mmoja kote Lebanoni, haswa katika maeneo yenye uwepo mkubwa wa wanachama wa Hezbollah. Milipuko hiyo ilijeruhi na kuua na kuzusha hofu.

Siku iliyofuata, redio za mawasilianoi zililipuka kwa njia hiyo hiyo, na kuua na kujeruhi mamia zaidi.

Wakati wa shambulio hilo, Israel na Hezbollah walikuwa wakirushiana makombora tangu Hezbollah ilipofyatua makombora kwenda Israel siku moja baada ya shambulio la Oktoba 7 la Hamas.

Miezi miwili baadaye, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alikiri kuwa Israel ilihusika.

Katika mahojiano na CBS, maajenti wawili wa zamani walifichua kuwa Mossad ilificha vilipuzi ndani ya betri zinazotumia vifaa hivyo vya mawasiliano.

Hezbollah walinunua bila kujua vifaa hivyo zaidi ya 16,000 kutoka kampuni feki miaka 10 iliyopita, na baadaye walinunua vifaa vingine 5,000, CBS iliripoti.

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Volker Turk alitaja shambulio hilo kuwa uhalifu wa kivita.

Kuuawa Mohsen Fakhrizadeh

A car with bullet holes in the windscreen

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Mossad inashukiwa kuhusika na mauaji ya mwanasayansi mkuu wa nyuklia wa Iran Mohsen Fakhrizadeh

Novemba 2020, msafara uliombeba Mohsen Fakhrizadeh, mwanasayansi mashuhuri wa nyuklia wa Iran, ulishambuliwa katika mji wa Absard, mashariki mwa mji mkuu, Tehran.

Fakhrizadeh aliuawa kwa kutumia bunduki iliyofyatuliwa kwa rimoti.

"Kutekeleza mauaji kwa njia kama hiyo dhidi ya mtu anayetembea bila ya raia yeyote kujeruhiwa kunahitaji akili," aliandika Jiyar Gol wa BBC Persian wakati huo.

Aprili 2018, Netanyahu alionyesha nyaraka kadhaa zinazodaiwa kuwa zinahusiana na mpango wa nyuklia wa Iran, ambazo alisema ziliibiwa miezi kadhaa hapo awali na Mossad katika operesheni kwenye kituo kilicho umbali wa kilomita 30 tu kutoka Tehran (hili lilithibitishwa baadaye na Rais wa Irani Hassan Rouhani).

Waziri mkuu wa Israel alimtaja Mohsen Fakhrizadeh katika kile alichosema ni mpango wa silaha za nyuklia ambao haujatangazwa.

"Dk Mohsen Fakhrizadeh ... kumbuka jina hilo," alisisitiza.

Hapo awali Iran iliishutumu Israel kwa kuwaua wanasayansi wengine wanne wa nyuklia wa Iran kati ya 2010 na 2012.

Kuuawawa Mahmoud al-Mabhouh

Mahmoud al-Mabhouh's images on a poster

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mahmoud al-Mabhouh alipigwa shoti ya umeme na kisha kunyongwa

2010, Mahmoud al-Mabhouh, kiongozi wa kijeshi wa Hamas, aliuawa katika hoteli ya Dubai.

Mwanzo ilionekana kama kifo cha kawaida, lakini polisi wa Dubai hatimaye waliweza kuitambua timu ya mauaji baada ya kuchunguza picha za CCTV.

Polisi baadaye walifichua kwamba al-Mabhouh aliuawa kwa shoti ya umeme na kisha kunyongwa.

Ilishukiwa kuwa operesheni hiyo ilipangwa na Mossad, na ilizua hasira ya kidiplomasia kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu.

Wanadiplomasia wa Israel, hata hivyo, walidai hakuna ushahidi unaohusisha Mossad na shambulio hilo.

Maujai ya Yahya Ayyash

Yahya Ayyash's photo on a billboard

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Picha ya Yahya Ayyash huonekana kwenye mabango kama ishara ya upinzani wa Palestina

1996, Yahya Ayyash, mtengenezaji mkuu wa mabomu wa Hamas, aliuawa kwa simu ya mkononi ya Motorola Alpha iliyojazwa gramu 50 za vilipuzi.

Ayyash, kiongozi mashuhuri katika tawi la kijeshi la Hamas, alisifika kwa utaalamu wake wa kutengeneza mabomu na kupanga mashambulizi tata dhidi ya Israel.

Mwishoni mwa 2019, Israeli iliondoa udhibiti wa baadhi ya taarifa juu ya mauaji hayo, na Channel 13 TV ya Israeli ilipeperusha rekodi ya mazungumzo ya simu ya mwisho ya Ayyash na baba yake.

Operesheni Brothers

A male Mossad agent stands next a Landrover full of Ethiopian Jews being smuggled from Sudan

Chanzo cha picha, Raffi Berg

Maelezo ya picha, Wakala wa Mossad amesimama karibu na gari lililojaa Wayahudi wa Ethiopia wanaosafirishwa kupitia Sudan

Mapema miaka ya 1980, Mossad - kwa maagizo ya Waziri Mkuu Menachem Begin - waliwasafirisha zaidi ya Wayahudi 7,000 wa Ethiopia hadi Israeli kupitia Sudan, kwa kutumia kituo bandia cha kupiga mbizi.

Sudan ilikuwa nchi, kwa hivyo Mossad walifanya kazi kwa siri, timu ya mawakala wa Mossad ilianzisha kituo cha mapumziko kwenye pwani ya Bahari ya Shamu upande wa Sudan.

Mchana, walijifanya kuwa wafanyakazi wa hoteli na usiku waliwasafirisha Wayahudi, ambao walisafiri kisiri kutoka nchi jirani ya Ethiopia, kwa ndege na bahari.

Operesheni hiyo ilifanyika kwa miaka mitano, na ilipogunduliwa, maajenti wa Mossad walikuwa tayari wameshaondoka.

Mauaji ya Munich

Members of the Israeli team march on the field of the Munich Olympic stadium on 6 September 1972 to attend the memorial ceremony paying tribute to their countrymen killed by Palestinian militants

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wachezaji wa timu ya Israel wakitembea katika uwanja wa Olimpiki wa Munich kuhudhuria hafla ya kumbukumbu ya wenzao waliouawa na wanamgambo wa Kipalestina.

1972, kikundi cha wanamgambo wa Palestina, Black September kiliwaua washiriki wawili wa timu ya Olimpiki ya Israel kwenye Michezo ya Olimpiki ya Munich na kuwakamata wengine tisa.

Wanariadha hao waliuawa baadaye katika jaribio la kuwaokoa lililofeli la polisi wa Ujerumani Magharibi.

Portraits of the eleven Israeli athletes and coaches slain in West Germany at the 1972 Olympic Games. They are (top left to right): Yosef Gutfreund, 40; Moshe Weinberg, 33: Yoseph Romano, 32; David Berger, 28; Mark Slavin, 18; Yaacov Springer, 52; (bottom left to right): Ze'ev Friedman, 28; Amitsur Shapira, 40; Eliezer Halfin, 24; Kehat Schorr, 53; Andre Spitzer, 27

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wanachama 11 wa timu ya Olimpiki ya Israeli ya 1972 waliuawa baada ya wapalestina wenye silaha kuvamia eneo lao.

Miaka iliyofuata, Mossad iliwalenga wale wanaoshukiwa kuhusika na shambulio hilo, akiwemo Mahmoud Hamshari.

Aliuawa na kilipuzi kilichotegwa kwenye simu katika nyumba yake mjini Paris.

Hamshari alipoteza mguu katika mlipuko huo na hatimaye kufariki dunia kutokana na majeraha yake.

Operesheni Entebbe

A woman is supported as she is led through crowds

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mateka wa ndege ya Entebbe waliachiliwa baada ya wiki moja kizuizini

Operesheni ya Entebbe nchini Uganda 1976 inachukuliwa kuwa moja ya misheni ya kijeshi yenye mafanikio zaidi ya Israeli.

Mossad ilitoa taarifa za kijasusi, huku jeshi la Israel likifanya operesheni hiyo.

Wanachama wawili wa chama cha Popular Front for the Liberation of Palestine na washirika wawili wa Ujerumani waliteka nyara ndege iliyokuwa inakwenda Paris na kuipelekeza Uganda. Waliwashika mateka abiria na wafanyakazi katika uwanja wa ndege wa Entebbe.

Makomando wa Israel walivamia uwanja wa ndege na kuwaokoa mateka 100 waliosalia wa Israel na Wayahudi.

Mateka watatu, watekaji nyara, wanajeshi kadhaa wa Uganda, na komando mkuu Yonatan Netanyahu (kaka ya Waziri Mkuu wa sasa wa Israel, Benjamin Netanyahu) waliuawa katika operesheni hiyo.

Afisa wa Nazi

Adolf Eichman behind a bar with a security official in uniform behind him

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Adolf Eichmann wakati wa kesi yake nchini Israel

Tukio la kutekwa nyara kwa afisa wa Nazi, Adolf Eichmann kutoka Argentina mwaka 1960 ni mojawapo ya mafanikio ya kijasusi ya Mossad.

Eichmann alihusika katika mauaji ya Holocaust, ambapo Wayahudi milioni sita waliuawa na Ujerumani ya Nazi katika Vita vya Pili vya Dunia.

Baada ya kukwepa kukamatwa kwa kuhama kati ya nchi kadhaa, hatimaye Eichmann aliishi Argentina.

Kundi la maajenti 14 wa Mossad walimfuatilia, wakamteka nyara, na kumpeleka Israel, ambako alishitakiwa na hatimaye kuuawa.

Opresheni zilizoshindwa

Licha ya oeresheni za Mossad kupangwa vyema, lakini si kila operesheni imefanikiwa.

Shambulio la Oktoba 7, 2023

A security official walks past tents and debris after the 7 October attack

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Takriban watu 1,200 waliuawa katika mashambulizi ya Hamas ya tarehe 7 Oktoba kusini mwa Israel

Shambulio lililoanzishwa na Hamas kwenye miji ya Israel karibu na mpaka wa Gaza tarehe 7 Oktoba 2023 liliishangaza nchi hiyo.

Kushindwa kwa Mossad kutabiri shambulio hilo kunachukuliwa kuwa kushindwa kukubwa.

Shambulio la Oktoba 7 lilisababisha mauaji ya watu wapatao 1,200, wengi wao wakiwa raia. Wengine 251 walichukuliwa Gaza kama mateka.

Katika kukabiliana na shambulio la Hamas, Israel ilianzisha vita kwenye Ukanda wa Gaza, hadi sasa vimesababisha vifo vya zaidi ya 55,000, wengi wao wakiwa ni raia, kulingana na Wizara ya Afya ya Gaza inayoendeshwa na Hamas.

Vita vya Yom Kippur

Two Israeli troops look across across the Suez Canal

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wanajeshi wa Israeli wakivuka Mfereji wa Suez wakati wa Vita vya 1973 vya Israel na nchi za Kiarabu

Karibu miaka 50 iliyopita. Tarehe 6 Oktoba 1973, Misri na Syria zilianzisha mashambulizi ya kushtukiza kwa Israeli ili kurejesha Peninsula ya Sinai na Milima ya Golan.

Wakati wa shambulio la Yom Kippur, siku takatifu zaidi katika kalenda ya Kiyahudi. Majeshi ya Misri yalivuka Mfereji wa Suez, na kupata hasara ndogo tu, huku majeshi ya Syria yakishambulia maeneo ya Israel na kupenya hadi kwenye milima ya Golan.

Umoja wa Kisovieti ulitoa vifaa kwa Syria na Misri, na Marekani ilitoa msaada wa dharura kwa Israel.

Israel iliweza kuviondoa vikosi hivyo na vita viliisha tarehe 25 Oktoba - siku nne baada ya azimio la Umoja wa Mataifa la kutaka mapigano yasitishwe.

Mahmoud al-Zahar

Mahmoud al-Zahar

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mahmoud al-Zahar's alikuwa mmoja wa viongozi wa Hamas waliokuwa wakisakwa sana na Mossad

Mwaka 2003, Israel ilifanya shambulizi la anga lililolenga nyumba ya kiongozi wa Hamas Mahmoud al-Zahar katika mji wa Gaza.

Ingawa al-Zahar alinusurika katika shambulio hilo, lilisababisha kifo cha mkewe na mwanawe, Khaled, pamoja na wengine kadhaa.

Shambulio hilo la bomu liliharibu kabisa makazi yake.

Khaled Meshaal

Khaled Meshaal speaking at a press conference

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Khaled Meshaal aliwahi kuwa kiongozi wa kisiasa wa Hamas kati ya 1996 na 2017

Katika operesheni iliyosababisha mzozo mkubwa wa kidiplomasia, Israel ilijaribu kumpa sumu Khaled Meshaal, mkuu wa ofisi ya kisiasa ya Hamas, huko Jordan mwaka 1997.

Misheni hiyo ilishindwa pale maajenti wa Israel walipokamatwa, na kuilazimisha Israel kutoa dawa ya kuokoa maisha ya Meshaali.

Mkuu wa wakati huo wa Mossad, Danny Yatom, aliruka kwa ndege hadi Jordan kumtibu Meshaal.

Tukio hilo lilivuruga kwa kiasi kikubwa uhusiano kati ya Israel na Jordan.

Lavon Affair

Egyptian President Gamal Abdel Nasser satnding and waving to a crowd

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Rais wa Misri Gamal Abdel Nasser akitangaza kutaifishwa kwa mfereji wa Suez

1954, Misri ilitibua operesheni ya kijasusi ya Israel iliyojulikana kama Operesheni Susannah.

Mpango huo ulikuwa wa kutega mabomu katika vituo vya Marekani na Uingereza nchini Misri kuishinikiza Uingereza kubakisha vikosi vyao vilivyowekwa kwenye Mfereji wa Suez.

Tukio hilo lilijulikana kwa jina la Lavon Affair, lililopewa jina la Waziri wa Ulinzi wa Israel wakati huo, Pinhas Lavon.

Inaaminika kuwa alihusika katika upangaji wa operesheni hiyo.