Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wenyeji Kenya wafuzu kwa fainali Cecafa baada ya kuwalaza Burundi
Wenyeji Kenya wamefuzu kwa michuano ya ubingwa wa kanda ya Afrika mashariki na kati, maarufu kama Cecafa Senior Challenge.
Kenya wamefuzu baada ya kufunga bao muda wa ziada dhidi ya Burundi katika nusu fainali iliyochezewa mjini Kisumu, Magharibi mwa Kenya Alhamisi.
Baada ya kumaliza dakika 90 bila bao, kiungo wa kati Whyvonne Isuza alifunga bao la ushindi kipindi cha kwanza muda wa kuongezwa.
Kenya, chini ya mkufunzi wao mpya Paul Put, sasa watacheza na mshindi wa nusufainali kati ya Uganda na Zanzibar kwenye fainali Jumapili.
Ushindi huo wa Kenya umeendeleza mwanzo mzuri kwa Mbelgiji Put ambaye alichukua usukani kama mkufunzi mkuu mwezi jana.