Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maafisa wa Urusi wakiri kuwepo kwa udanganyifu
Kwa mara ya kwanza, Maafisa wa Urusi wamekiri kuwepo kwa mipango ya matumizi ya dawa zilizoharamishwa iliyoathiri mashindano makubwa duniani.
Ripoti iliyotolewa mnamo tarehe 9 Disemba, ilisema kuwa zaidi ya wanamichezo 1,000 wa Urusi walinufaika na udanganyifu kati ya mwaka wa 2011 na 2015.
Kwenye mahojiano na jarida la New York times, maafisa walikiri mpango huo lakini wakapinga kwamba ilidhaminiwa na serikali.
"Ilikuwa ni mikakati iliyopangwa," amesema Anna Antseliovich, kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka kuu ya kuchunguzi matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Urusi