Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Bolt anyakua dhahabu mbio za mita 200 Olimpiki Rio
Mwanariadha Mjamaica Usain Bolt ameshinda mbio za mita 200 katika michuano ya Olympics huko Rio nchini Brazil na kujinyakulia medali ya dhahabu ya pili baada ya kunyakua ya michuano ya mbio za mita 100.
Ameshinda kwa kirahisi mbio hizo za mita 200 kwa kutumia sekunde 19.79. Bolt kwa sasa anahitaji kushinda mbio za mita 4x 100 za kupokezana vijiti ili kukamilisha medali ya tatu ya dhahabu kama alivyofanya katika michuano iliyopita.
Mapema wiki hii alidhihirisha kuwa ni mwamba wa mbio fupi pale aliposhinda mbio za mita 100 na kunyakuwa medali ya dhahabu.
Katika matokeo mengine Marekani imenyakulia medali nyingine nne za dhahabu ikiwemo ya mwanariadha wake Ashton Eaton.