Rubio: Tuliishambulia Iran kwa sababu Israel ilikuwa karibu kushambulia na majeshi yetu yalikuwa hatarini
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio amesema katika akaunti mpya sababu ya kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran.
Anasema kwamba Marekani ilipata taarifa kutoka kwa Israel kwamba ilikuwa inapanga mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran, .
Washington imedai kwamba hatua hiyo ya Israel inaambatana na shambulio la mara moja la Iran dhidi ya majeshi ya Marekani, na kwa hiyo jeshi la Marekani lilianzisha operesheni ya kijeshi dhidi ya Iran kwa lengo la kuizuia.
Pia aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba "dhamira" ya msingi ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran ni "kuharibu uwezo wao wa makombora ya balistiki ya [Wairani] wa kuyajenga pamoja na tishio ambalo jeshi lao la majini linaleta kwa meli za kimataifa."
Aliendelea kusema kuwa anatumai watu wa Iran wanaweza "kuiangusha" serikali hii na "kujenga mustakabali mpya wa nchi yao."
Bw. Rubio aliongeza kuwa "tungefurahi kama hili lingewezekana," lakini akasisitiza kuwa "lengo la misheni hii ni kuharibu uwezo wao wa makombora ya balistiki na uwezo wao wa majini."
Viongozi wa Israel nao wameeleza kuwa "kupinduliwa kwa utawala wa Jamhuri ya Kiislamu" ni moja ya malengo makuu ya mashambulizi yao ya pamoja na Marekani.
Bw. Rubio, ambaye pamoja na wadhifa wake wa Waziri wa Mambo ya Nje pia ni mshauri mkuu wa usalama wa taifa wa Donald Trump, alienda kwenye Bunge la Congress la Marekani Jumatatu ili kuwaeleza wawakilishi na maseneta wa Marekani sababu za kuanzisha vita na Iran.