Moja kwa moja, Ubalozi wa Marekani Saudi Arabia washambuliwa na ndege zisizo na rubani

Wizara ya Ulinzi ya Saudi Arabia imethibitisha kwamba ubalozi wa Marekani mjini Riyadh ulishambuliwa na ndege mbili zisizo na rubani.

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

  1. Watu wasiopungua 169 wauawa katika shambulio la 'kushtukiza' Sudani Kusini

    Silaha

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Mamlaka nchini Sudan Kusini zimesema watu wasiopungua 169, wakiwemo maafisa wakuu, waliuawa Jumapili wakati kundi la watu wasiojulikana walipoanzisha shambulio katika eneo moja kaskazini mwa nchi.

    Akielezea shambulio hilo linalodaiwa kufanywa na vijana kadhaa wenye silaha, Waziri wa Habari wa Eneo la Utawala la Ruweng, James Monyluak Mijok, alidai kwamba walitoka katika jimbo jirani la Unity na walikuwa na uhusiano na Jeshi la Ukombozi wa Watu wa Sudan katika Upinzani (SPLA-IO).

    SPLA-IO imekana kuhusika kokote katika shambulio hilo, ikishutumu mamlaka ya jimbo la Unity kwa kuingilia vurugu hizo kisiasa.

    Umoja wa Mataifa umeonya mara kwa mara kwamba nchi iko katika hatari ya kurudi kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    “Waliokufa ni pamoja na watoto 90, wanawake na wazee, pamoja na maafisa 79 wa vikosi vya kikanda, wakiwemo polisi,” Mijok alisema.

    Mijok aliiambia BBC kwamba washambuliaji waliingia kaunti ya Abiemnom katika eneo la Ruweng kabla ya alfajiri Jumapili, takribani saa 4:30 asubuhi kwa saa za huko (02:30 GMT), wakati watu bado walikuwa wamelala na “waliwashitukiza”.

    Alisema kuwa vikosi vya serikali vilivyokuwa eneo la tukio “vilizidiwa idadi… Washambuliaji walichoma moto nyumba na masoko wakati wa mapigano yaliyodumu kati ya saa tatu hadi nne.” Maafisa kadhaa waandamizi wa eneo hilo waliuawa, akiwemo kamishna wa kaunti na mkurugenzi mtendaji.

    Mijok alisema tangu wakati huo vikosi vya serikali vimewafurkuza washambuliaji na kwamba sasa mamlaka zina udhibiti kamili wa eneo hilo.

    Unaweza kusoma;

  2. Netanyahu adai kuwa ingekuwa vigumu kwa mpango wa nyuklia wa Iran kudhibitiwa

    Netanyahu

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ametetea mashambulizi ya kijeshi ya Israel dhidi ya Iran, akidai kwamba ongezeko la hivi karibuni la mpango wa nyuklia wa Tehran “lisingekuwa rahisi kudhibiti ndani ya miezi michache” kabla ya hatua ya Israel.

    Licha ya mashambulizi ya pamoja ya anga ya Israel na Marekani yaliyolenga vituo vitatu vya nyuklia wakati wa vita vya siku 12 mwezi Juni, Netanyahu anasema wanajeshi na mafundi wa Iran walianza kujenga maeneo mapya, yakiwemo “ya chini ya ardhi,” ambako wangeweza kuendeleza makombora ya balistiki na mabomu ya atomiki.

    “Kama hakuna hatua ingechukuliwa sasa, basi hakuna hatua ambayo ingeweza kuchukuliwa baadaye,” Netanyahu aliiambia Fox News.

    Israel kwa muda mrefu imepinga urutubishaji wa nyuklia wa Iran, ikionya kuwa unaweza kutumika kutengeneza silaha za nyuklia badala ya kutumika kwa madhumuni ya amani kama inavyodai serikali ya Iran.

    Unaweza kusoma;

  3. Ubalozi wa Marekani Saudi Arabia washambuliwa na ndege zisizo na rubani

    Athari za mashambulizi

    Chanzo cha picha, Reuters

    Wizara ya Ulinzi ya Saudi Arabia imethibitisha kwamba ubalozi wa Marekani mjini Riyadh ulishambuliwa na ndege mbili zisizo na rubani, kulingana na makadirio ya awali.

    Katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X, wizara hiyo ilisema hii ilisababisha "moto mdogo na uharibifu mdogo wa vifaa kwenye jengo hilo".

    Ubalozi wa Marekani umewaagiza wafanyakazi wake walioko Saudi Arabia kubaki ndani katika miji ya Jeddah, Riyadh, na Dhahran kutokana na uwezekano wa tishio la kiusalama.

    Ujumbe huo utapunguza au utaepuka safari zisizo za lazima kwenda kwenye vituo vya kijeshi katika eneo hilo, kama tahadhari kwa sababu za usalama.

    Donald Trump alikiambia kituo cha runinga cha NewsNation kwamba Marekani italipiza kisasi “hivi karibuni” kufuatia shambulio dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Riyadh na vifo vya wanajeshi wa Marekani.

    Wanajeshi sita wa Marekani wameuawa hadi sasa huku 18 wakiwa wamejeruhiwa, Marekani ilisema Jumatatu usiku.

    Unaweza kusoma;

  4. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu hii leo