Watu wasiopungua 169 wauawa katika shambulio la 'kushtukiza' Sudani Kusini

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Mamlaka nchini Sudan Kusini zimesema watu wasiopungua 169, wakiwemo maafisa wakuu, waliuawa Jumapili wakati kundi la watu wasiojulikana walipoanzisha shambulio katika eneo moja kaskazini mwa nchi.
Akielezea shambulio hilo linalodaiwa kufanywa na vijana kadhaa wenye silaha, Waziri wa Habari wa Eneo la Utawala la Ruweng, James Monyluak Mijok, alidai kwamba walitoka katika jimbo jirani la Unity na walikuwa na uhusiano na Jeshi la Ukombozi wa Watu wa Sudan katika Upinzani (SPLA-IO).
SPLA-IO imekana kuhusika kokote katika shambulio hilo, ikishutumu mamlaka ya jimbo la Unity kwa kuingilia vurugu hizo kisiasa.
Umoja wa Mataifa umeonya mara kwa mara kwamba nchi iko katika hatari ya kurudi kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.
“Waliokufa ni pamoja na watoto 90, wanawake na wazee, pamoja na maafisa 79 wa vikosi vya kikanda, wakiwemo polisi,” Mijok alisema.
Mijok aliiambia BBC kwamba washambuliaji waliingia kaunti ya Abiemnom katika eneo la Ruweng kabla ya alfajiri Jumapili, takribani saa 4:30 asubuhi kwa saa za huko (02:30 GMT), wakati watu bado walikuwa wamelala na “waliwashitukiza”.
Alisema kuwa vikosi vya serikali vilivyokuwa eneo la tukio “vilizidiwa idadi… Washambuliaji walichoma moto nyumba na masoko wakati wa mapigano yaliyodumu kati ya saa tatu hadi nne.” Maafisa kadhaa waandamizi wa eneo hilo waliuawa, akiwemo kamishna wa kaunti na mkurugenzi mtendaji.
Mijok alisema tangu wakati huo vikosi vya serikali vimewafurkuza washambuliaji na kwamba sasa mamlaka zina udhibiti kamili wa eneo hilo.
Unaweza kusoma;


