Iran: Marekani ilipe fidia kamili kutokana na Shambulio la Israel

Chanzo cha picha, Getty Images
Balozi wa kudumu wa Iran katika umoja wa mataifa UN Amir Saeed Irvani,ameomba fidia na marekebisho kutoka kwa Marekani kwa waathiriwa,majeruhi na uharibifu uliosababishwa katika taifa lake,kupitia barua yake kwa baraza la usalama.
Katika barua yake Balozi Irvani alitaja taarifa ya hivi karibuni ya rais Trump kama sababu ya kuhusika kwake moja kwa moja na mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran akisema
“Marekani na Israel zinawajibika kikamilifu na kwa pamoja kwa vitendo vyao vya uchokozi na matokeo yanayotokana navyo dhidi ya Iran.”
Aidha Irvani aliandika kwamba Donald Trump alieleza katika mkutano na vyombo vya Habari November 6 kwamba alikuwa na “udhibiti kamili” wa shambulio la Israel dhidi ya Iran.
Aidha Balozi Irvani pia anazitaja kauli za Trump kuwa tata na kukinzana na za Waziri wa ulinzi wa Marekani Mark Rubio,ambaye 13 June alikanusha Marekani kuhusika katika shambulizi la Israel dhidi ya Iran.
Soma Zaidi:











