Mamlaka ya Hali ya Hewa Kenya yatoa tahadhari ya mafuriko
Wakenya wameshauriwa kujiandaa kwa mvuu kubwa itakayonyesha katika maeneo tofauti nchini hadi Jumamosi.
Kulingana na taarifa iliyotolewa kwa umma na Idara ya utabiri wa hali ya hewa mvua itakayozidi milimita 20 itaendelea kunyesha katika maeneo tofauti nchini ndani ya saa 24 zijazo.
Maeneo yatakayoshuhudia mvua kubwa ni pamoja na Kanda ya Ziwa Victoria, Magharibi mwa Kenya, nyanda za juu na kati pamoja na nyanda za chini kusini.
Maeneo ya Pwani yanatarajia kupata mvua kubwa hadi tarehe tisa mwezi Machi.
Wakaazi wa maeneo yaliyotajwa wametahadharishwa kwamba mvua hizo huenda zikasababisha mafurika.
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa mafurika yanaweza kushahudiwa hata katika maeneo ambayo hayatakuwa na mvua kubwa.
Mvua kubwa ikiandamana na nguromo za radi imekuwa ikinyesha katika maeneo tofauti ya nchi katika wiki za hivi karibuni hasa nyakati za usiku.
Msimu wa mvua wa wa mwezi Machi na Mei umeanza katika maeneo ya Nyanda za Juu Magharibi mwa Bonde la Ufa, Bonde la Ziwa Victoria, maeneo ya kati mwa nchi na kusini mwa bonde la ufa.
Wakenya wameombw akuwa makini msimu huu wa mvua na kutoendesha magari katika barabara zilizofurika maji.
Pia unaweza kusoma: