Tetesi za soka Ulaya Alhamisi: Real Madrid yajiondoa katika harakati za kumsajili Rodri

Muda wa kusoma: Dakika 2

Real Madrid wamejiondoa katika kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Manchester City Rodri, moja ya sababu ikiwa ni kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania mwenye umri wa miaka 29 anaweza kugharimu angalau euro 60m (£52m). (Sport - In Spanish)

Meneja wa Bournemouth Andoni Iraola anafikiria kusaini kandarasi mpya katika klabu hiyo licha ya kutakiwa na Crystal Palace na Tottenham. (Mail - Subscription Required)

Kiungo wa kati wa zamani wa Tottenham na Uingereza Dele Alli, 29, amerejea katika mazoezi na Spurs huku akitafuta kurejea katika soka baada ya kuondoka katika klabu ya Como ya Italia mwezi Septemba. (Standard)

Crystal Palace wamemuongeza kocha wa zamani wa Tottenham Thomas Frank kwenye orodha ya makocha wanaotarajiwa kuchukua nafasi ya Oliver Glasner anayeondoka. (Sun)

Real Madrid wanafikiria kumbadilisha meneja Alvaro Arbeloa na kuchukua nafasi ya kocha mkuu wa AC Milan Massimiliano Allegri msimu ujao. (Corriere dello Sport - In Italy)

Arsenal, Liverpool na Manchester United wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Juventus na Ufaransa Khephren Thuram, 24. (CaughtOffside)

Mshambulizi wa Ufaransa Antonie Griezmann, 34, anakabiliwa na uamuzi wa kusalia Atletico Madrid au kukubali ofa ya kujiunga na klabu ya Orlando City inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka. (Footmercato - In French)

Bayern Munich wanafikiria kwa dhati kumnunua mshambuliaji wa Galatasaray na Nigeria Victor Osimhen, 27, huku wakitarajia kujiandaa na kuondoka kwa mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 32. (Footmercato - In French)

Klabu ya Ujerumani RB Leipzig itataka takriban euro 80m (£70m) ikiwa wanataka kumuuza winga wa Ivory Coast Yan Diomande, 19, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool na Manchester United miongoni mwa wengine. (Football Insider)

Liverpool wameelekeza mawazo yao kwa Diomande kwa kuwa hawaamini kuwa wataweza kumsajili winga wa Ufaransa Michael Olise kutoka Bayern Munich, ambaye anataka kuongeza mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 zaidi ya 2029. (Sky Sports Germany)

Hatimaye Hearts wanaweza kudai pauni milioni 2 kutoka kwa Keir McMeekin mwenye umri wa miaka 16 kwa uhamisho uliokaribia kwenda Manchester City, huku kiungo huyo wa kati wa Scotland chini ya miaka 17 akiwa tayari kusaini makubaliano ya awali ya kandarasi kabla ya kuhamia katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza. (Mail).