Moja kwa moja, Bunge la Seneti Marekani lashindwa kudhibiti nguvu za kivita za Trump huku Iran ikiishambulia Israel

Hatua hiyo ingesitisha hatua za kijeshi za Marekani nchini Iran bila idhini ya bunge.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Urusi yaishutumu Ukraine baada ya meli yake kuzama katika bahari ya Mediterania

    Picha ambazo hazijathibitishwa za moto huo ziliwekwa mtandaoni na Mshauri wa Waziri wa Ulinzi wa Ukraine

    Chanzo cha picha, Serhii Sternenko/X

    Maelezo ya picha, Picha ambazo hazijathibitishwa za moto huo ziliwekwa mtandaoni na Mshauri wa Waziri wa Ulinzi wa Ukraine

    Meli ya Urusi ya gesi ya kimiminika (LNG) imezama katika bahari ya Mediterania kati ya Libya na Malta baada ya kukumbwa na mlipuko na kuwaka moto, maafisa wa bandari ya Libya wamesema.

    Urusi imeishutumu Ukraine kwa kuishambulia Arctic Metagaz kwa "ndege zisizo na rubani" zilizorushwa kutoka pwani ya Libya.

    Idara ya usalama ya serikali ya Ukraine SBU haijatoa kauli yoyote kuhusiana na madai hayo huku mamlaka ya bandari ya Libya imesema chanzo cha moto kwenye meli hiyo hakijabainika.

    Raia wa Libya wanasema meli hiyo ilikuwa imebeba takriban tani 62,000 za LNG kabla ya kukumbwa na milipuko na kwamba ilizama takriban maili 130 (240km) kaskazini mwa bandari ya Sirte nchini Libya.

    Wizara ya uchukuzi ya Urusi ilisema Warusi 30 walikuwa ndani ya Arctic Metagaz.

    Waziri wa Mambo ya Ndani wa Malta Byron Camilleri alisema wote walipatikana wakiwa "salama katika boti ya uoko" wakati wa operesheni ya uokoaji ya vikosi vya jeshi vya Malta.

    Picha ambazo hazijathibitishwa zilizoibuka mitandaoni zinaonekana kuonyesha meli hiyo ikiwaka moto baada ya shambulio hilo la Jumanne.

    Maelezo zaidi:

  2. Zelensky tayari kuzisaidia nchi za Ghuba kukabiliana na mashambulizi ya droni

    Volodymyr Zelensky

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky

    Rais Volodymyr Zelensky amesema kwamba Ukraine inaandaa mipango ya kupeleka wataalamu katika eneo la Ghuba kusaidia washirika walinda nchi zao dhidi ya ndege zisizo na rubani na makombora ya Iran.

    Anasema alizungumza na wenzao katika Falme za Kiarabu UAE na Qatar hapo jana, na Jordan na Bahrain hii leo.

    Baada ya kujadili mzozo wa Mashariki ya Kati na mawaziri na makamanda, aliwaomba kubuni mkakati wa kuwasaidia washirika - bila kudhoofisha ulinzi wa Ukraine yenyewe.

    Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa X, Rais Zelensky alisema: "Ukraine inaweza kusaidia kulinda maisha na kuleta utulivu..."

    Aliongeza: "Jeshi letu lina uwezo unaohitajika. Wataalamu wa Ukraine watafanya kazi mashinani, na timu tayari zinaratibu hili. Tuko tayari kusaidia kulinda maisha, kulinda raia, na kuunga mkono juhudi za kweli za kuleta utulivu wa hali hiyo na kurejesha urambazaji salama katika eneo hilo."

    Soma pia:

  3. EPL: Arsenal yatamba, City wapata sare huku Man United ikipoteza

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Arsenal walinusurika pambano kali dhidi ya Brighton na kuendeleza uongozi wao kileleni mwa Ligi ya Premia hadi pointi saba.

    Brighton walikuwa timu bora kwa muda mrefu - lakini bao la Bukayo Saka lililofungwa mapema lilitosha kukipa kikosi cha Mikel Arteta ushindi wa hali ya juu huku wapinzani wao Manchester City wakilazimishwa sare ya 2-2 nyumbani na Nottingham Forest.

    Usiku wa Arsenal nusura uanze kwa njia ya janga katika sekunde za mwanzo wakati kipa David Raya alipompatia mpira kimakosa Carlos Baleba, lakini jaribio lake la kupangua lilikuwa dhaifu, na kumruhusu Gabriel kurudi nyuma na kuokoa shambulizi lake.

    Baadaye bahati ya The Gunners ilisimama baada ya dakika tisa wakati shuti la kawaida la Saka lilipomtoka Baleba na kupita kwenye miguu ya kipa wa Brighton Bart Verbruggen, ambaye hakuwa na jibu.

    Wakati huohuo Nattingham ambao walikuwa wanacheza ugenini dhidi ya Man City walikaa nyuma na kulinda lango la huku City ikitawala katika kipindi kirefu cha mchezo kabla ya Antoine Semenyo kufunga bao la kwanza na kutoa onyo kwa wageni.

    Wenyeji waliweka presha yao baada ya nusu saa wakati Rayan Cherki alipozamisha krosi ndani ya eneo la hatari na aliyesajiliwa Januari Semenyo akafunga bao lake la saba tangu ajiunge na City.

    Vilevile Manchester United ililazimika kukubali matokeo baada ya kufungwa 2-1 na wachezaji 10 wa Newcastle ugenini.

    Hatahivyo Michael Carrick hakuitupa timu yake tofauti na mtangulizi wake Ruben Amorim ambaye mara nyengine alinukuliwa akisema : "hii labda ni timu mbaya zaidi katika historia ya Manchester United", wakati alipokuwa akitoa maoni hayo zaidi ya mwaka mmoja uliopita baada ya kushindwa nyumbani na Brighton.

    Lakini Carrick anajua siku 11 kati ya kichapo cha 2-1 kutoka kwa Newcastle katika uwanja wa St James' Park na ziara ya Aston Villa Old Trafford mnamo Machi 15 zinaweza kuwa muhimu zaidi msimu wake.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Hezbollah 'haitajisalimisha' asema kiongozi wake huku mashambulizi ya Israel yakiongezeka

    Kiongozi wa Hezbollah Naim Qassem pichani Julai 2024

    Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images

    Maelezo ya picha, Kiongozi wa Hezbollah Naim Qassem

    Kiongozi wa Hezbollah Naim Qassem amesema Kundi hilo linaloungwa mkono na Iran "halitajisalimisha" huku vita na Israel vikiendelea kuongezeka.

    Katika hotuba yake ya kwanza ya hadhara tangu mzozo wa kikanda kuenea nchini Lebanon siku ya Jumatatu, Qassem alisema Hezbollah ilizingatia makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwishoni mwa 2024, lakini Israel "haikuzingatia masharti yake yoyote".

    "Tulikubaliana na suluhisho la kidiplomasia tukiliona kuwa ni fursa kwa serikali kuchukua jukumu lake, lakini tumekuwa tukisema mara kwa mara 'kuna mipaka ya uvstahamilivu'," alisema katika hotuba ya runinga.

    "Chaguo letu ni kukabiliana nao hadi kufikia hatua ya kujitolea kabisa, kwa mipaka ya mbali zaidi, na hatutasalimu amri," alisema.

    Hezbollah ilirusha roketi na ndege zisizo na rubani kuelekea Israel siku ya Jumatatu baada ya Kiongozi Mkuu wa Iran Ayotollah Ali Khamenei kuuawa katika mashambulizi ya Marekani na Israel.

    Israel imejibu mashambulizi ya anga na kupeleka wanajeshi kusini mwa Lebanon, huku maelfu ya raia wakilazimika kutoroka makaazi yao.

    Maelezo zaidi:

  5. Bunge la Seneti la Marekani lashindwa kudhibiti mamlaka ya vita ya Trump dhidi ya Iran

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Azimio la pande mbili linalolenga kudhibiti uwezo wa Rais Donald Trump wa kuanzisha vita nchini Iran limeshindwa katika Bunge la Seneti la Marekani, huku mgogoro ukiendelea kuongezeka Mashariki ya Kati.

    Hatua ya mamlaka ya vita ilikataliwa kwa kura 53 dhidi ya 47 ambayo kwa kiasi kikubwa kilipigwa kwa misingi ya chama. Ingesitisha hatua za kijeshi za Marekani nchini Iran bila idhini ya bunge.

    Wabungue wa chama cha Democratic wanasema kuwa Trump alichukua hatua ya kuishambulia Iran bila idhini ya Congress kwa kutoa sababu zinazobadilika za vita. Baadhi ya wa Republican wanasema watazuia azimio hilo, lakini wanaweza kubadilisha msimamo wao ikiwa vita vitaongezeka.

    Huku hayo yakijiri Jeshi la Israel limefanya mashambulizi mengine dihdi ya mkuu wa Iran Tehran.

    "IDF imeanza wimbi la ziada la mashambulizi yanayolenga miundombinu ya kijeshi ya utawala wa Iran kote Tehran," Jeshi la Ulinzi la Israel linasema katika taarifa.

    Jeshi hilo halikutoa maelezo zaidi kuhusu eneo mahususi, lakini inasema maelezo zaidi yatafuata.

    Shirika la habari la AFP linaripoti kuwa waandishi wake walishuhudia mlipuko mkubwa katika mji mkuu Jumatano usiku.

    Hapo awali, jeshi la Israel lilitangaza kuwa jeshi lake la anga lilikuwa limekamilisha "mashambulio makubwa" dhidi ya kambi ya mashariki ya Tehran yenye vituo vya amri na maafisa wa usalama wa ndani.

    Soma zaidi:

  6. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja.