Jeshi Iran laapa kulinda mali ya umma huku ikijaribu kutuliza ghasia zinazoongezeka

Chanzo cha picha, Middle East Images / AFP via Getty Images
Jeshi la Iran limesema siku ya Jumamosi kwamba litalinda miundombinu ya kimkakati na mali ya umma na kuwasihi Wairani kuzuia "njama za adui", huku taasisi ya makasisi ikiongeza juhudi za kuzima maandamano makubwa zaidi nchini humo kuwahi kutokea.
Taarifa hiyo ya kijeshi ya Iran ilikuja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutoa onyo jipya kwa viongozi wa Iran siku ya Ijumaa, na baada ya Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio siku ya Jumamosi kutangaza kuwa: "Marekani inawaunga mkono watu jasiri wa Iran."
Ghasia kutokana na maandamano zimeendelea usiku kucha. Vyombo vya habari vya serikali vilisema jengo la manispaa lilichomwa moto huko Karaj, magharibi mwa Tehran, na kuwalaumu "waasi".
Soma zaidi:







