Israel yasema imewashambulia viongozi wakuu wa Hamas huku milipuko ikisikika huko Doha

Milipuko imesikika na moshi umeonekana ukipanda juu ya mji mkuu wa Qatar Doha, shirika la habari la AFP na ripoti ya Reuters.

Muhtasari

  • Video yaonyesha jengo lililoharibiwa baada ya Israel kuwalenga viongozi wa Hamas nchini Qatar
  • Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani 'ukiukaji mkubwa' wa Israel kwa mamlaka ya Qatar
  • Ikulu ya White House imethibitisha kuwa iliarifiwa kuhusu shambulio la Israel
  • Netanyahu alikuwa katika makao makuu ya shirika la usalama la Israel wakati wa shambulio hilo
  • Maswali mazito kuhusu shambulio la Israel Qatar
  • Harambee Stars yaicharaza bila jibu Ushelisheli
  • Zaidi ya watu 20 waliuawa katika shambulio la Urusi huko Ukraine, Zelensky asema
  • Zelensky: Putin anataka "kuichukua Donbass" ifikapo mwisho wa mwaka
  • ICC yafungua kesi ya uhalifu wa kivita dhidi ya kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony
  • Putin amtunuku Jenerali Gerasimov, mwanajeshi mkuu wa Urusi, medali ya 'ujasiri'
  • Wabunge wa Marekani watoa 'kitabu cha siku ya kuzaliwa' cha Epstein chenye madai ya saini ya Trump
  • Ufaransa katika mzozo mpya wa kisiasa baada ya wabunge kumtimua waziri mkuu
  • Israel yafanya uvamizi viungani mwa miji ya na Homs na Latakia nchini Syria

Moja kwa moja

Na Dinah Gahamanyi

  1. Ripoti zinaonyesha mpatanishi mkuu wa Hamas miongoni mwa walengwa

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Kulia ni Khalil al-Hayya, mpatanishi mkuu wa masuala ya Gaza

    Kama tulivyoripoti, afisa wa Hamas anatuambia kwamba wanachama wa timu yao ya mazungumzo walilengwa wakati wa mkutano.

    Maelezo zaidi sasa yanaanza kujitokeza.

    Afisa wa ngazi ya juu wa Israel anaviambia vyombo vya habari vya Israel kwamba wanachama wa Hamas waliolengwa ni pamoja na Khalil al-Hayya, mpatanishi mkuu wa Gaza aliye uhamishoni, na Zaher Jabarin, kiongozi wa Ukingo wa Magharibi aliye uhamishoni.

    "Tunasubiri matokeo ya mashambulizi. Kuna maelewano kati ya uongozi wa kisiasa na usalama," afisa huyo anaongeza.

    Siku ya Jumatatu, Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz alikuwa amewaonya viongozi wa Hamas wanaoishi nje ya nchi kwamba wanakabiliwa na "maangamizi" na Gaza itaangamizwa ikiwa kundi hilo halitawaachilia mateka wake na kuweka silaha zake chini.

    Jeshi la Israel lilianzisha kampeni huko Gaza kujibu shambulio lililoongozwa na Hamas kusini mwa Israel tarehe 7 Oktoba 2023, ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 251 wakichukuliwa mateka.

    Takriban watu 64,605 ​​wameuawa katika mashambulizi ya Israel huko Gaza tangu wakati huo, kulingana na wizara ya afya ya eneo hilo inayoendeshwa na Hamas.

  2. Habari za hivi punde, Mataifa ya kiarabu yalaani shambulio la Israel dhidi ya mji mkuu wa Qatar

    Tumeona hisia kutoka kwa nchi zinazozunguka Mashariki ya Kati, zikitoa lawama kufuatia shambulio la Israel dhidi ya maafisa wa Hamas katika mji mkuu wa Qatar, Doha. Jordan imelaani "kwa maneno makali", shambulio la Israel huko Qatar.

    Wizara yake ya mambo ya nje inaeleza kuwa ni "kuenea kwa uchochezi hatari na kutokubalika".

    Katika hisia sawa, Kuwait imeelezea "kulaani vikali na kukemea" shambulio hilo. Abdullah bin Zayed, naibu waziri mkuu wa UAE, pia amelaani vikali shambulio hilo.

    Sultani wa Oman, katika taarifa kutoka kwa wizara ya mambo ya nje ya Oman, ameelezea shambulio hilo kama "ukiukaji wa wazi wa uhuru".

  3. Netanyahu anasema shambulio hilo lilitokana na ufyatuaji risasi wa Oktoba 7 mjini Jerusalem

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Taarifa ya pamoja ya Benjamin Netanyahu na Waziri wake wa Ulinzi Israel Katz inasema kuwa kufuatia mashambulizi ya Jerusalem na Gaza, waziri mkuu wa Israel aliviagiza vyombo vyake vya usalama kujiandaa kuulenga uongozi wa Hamas.

    Inasema kwamba alasiri ya leo iliwasilisha fursa ya kufanya kazi na, kwa kuungwa mkono kikamilifu na viongozi wa ulinzi wa Israeli, wawili hao kwa pamoja waliamua kushambulia .

    Inaongeza kuwa IDF na Shin Bet waliarifiwa kuhusu mipango ya shambulio hilo jana usiku.

    Taarifa hiyo inaendelea kuwa Netanyahu na Katz wanaamini kuwa shambulio hilo lilikuwa halali kutokana na uongozi wa Hamas kuwa nyuma ya shambulio la Oktoba 7, 2023 na ufyatuaji risasi mjini Jerusalem jana.

    Mapema leo, Hamas ilidai kuhusika na shambulizi hilo lililosababisha vifo vya Waisrael sita na wengine kadhaa kujeruhiwa.

  4. Habari za hivi punde, Haijulikani ni viongozi wangapi wa Hamas, ambao bado wako hai

    Ripoti kutoka Doha zilizungumza kuhusu milipuko minane tofauti, huku moshi mwingi ukipanda juu ya jiji hilo.

    Ndani ya dakika chache, Israeli iletekeleza mashambulizi; jeshi likisema lilitekeleza shambulio sahihi lililolenga uongozi mkuu wa Hamas.

    Israel iliianzisha, ikaiendesha na inachukua jukumu kamili, Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alichapisha kwenye mitandao ya kijamii.

    Aliiita operesheni huru kabisa ya Israeli, akijibu labda kwa ripoti za vyombo vya habari vya Israeli kwamba Washington inaweza kuwa imefahamishwa na kutoa rukhusa .

    Huko Doha, serikali ya Qatar ilijibu kwa hasira, ikilitaja shambulio hilo kuwa la kizembe na la woga, na ukiukaji wa wazi wa sheria na kanuni za kimataifa.

    Kauli kama hizo za hasira zilitoka katika ulimwengu wa Kiarabu.

    Shambulio hilo linajiri siku mbili tu baada ya utawala wa Trump kutangaza mapendekezo yake ya hivi punde ya kumaliza vita huko Gaza.

    Kuna uwezekano viongozi wa Hamas walikuwa wanakutana kwa usahihi kuzijadili.

    Huku ripoti zikiendelea kutoka eneo la tukio, haijulikani ni wangapi kati yao, ikiwa wapo, ambao bado wako hai.

  5. Video yaonyesha jengo lililoharibiwa baada ya Israel kuwalenga viongozi wa Hamas nchini Qatar

    .

    Chanzo cha picha, X

    Maelezo ya picha, .Jumba lililoshambuliwa na

    BBC Verify imechapisha eneo la mlipuko katika mji mkuu wa Qatar Doha kufuti shambulio la Israel lililolenga uongozi mkuu wa Hamas.

    Kwa kutumia picha za satelaiti na picha za Taswira ya Mtaa ya Google, tumethibitisha kanda inayoonyesha moshi ukipanda kutoka sehemu iliyoharibiwa sana ya jengo lililo karibu na kituo cha mafuta cha Woqod kwenye Mtaa wa Wadi Rawdan, karibu na wilaya ya West Bay Lagoon kaskazini mwa Doha ya kati.

  6. Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani 'ukiukaji mkubwa' wa Israel kwa mamlaka ya Qatar

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani "ukiukaji huu wa wazi wa uhuru na uadilifu wa eneo la Qatar".

    Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari muda mfupi uliopita, amesema alikuwa amearifiwa kuhusu shambulio hilo dhidi ya Qatar, ambalo analielezea kama "nchi ambayo imekuwa na jukumu chanya kufikia usitishaji mapigano na kuachiliwa kwa mateka wote".

    "Pande zote lazima zifanye kazi ili kufikia usitishaji vita wa kudumu, sio kuuangamiza," mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa anasema.

  7. Ikulu ya White House imethibitisha kuwa iliarifiwa kuhusu shambulio la Israel

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Rais Donald Trump

    Afisa wa Ikulu ya White House ameithibitishia BBC kwamba utawala wa Trump "uliarifiwa" kuhusu shambulio la Israel dhidi ya Doha kabla ya kufanyika.

    Shambulio la Israel dhidi ya Qatar, mshirika mkuu asiye wa Nato kwa Marekani, mara moja lilizua maswali kuhusu kiwango cha ufahamu na ushiriki wa Marekani, hasa kutokana na takriban wanajeshi 10,000 wa Marekani walioko nchini humo.

    Tuna uwezekano wa kusikia zaidi kutoka kwa mtazamo wa Ikulu saa 18:00 BST wakati Katibu wa Vyombo vya Habari Karoline Leavitt atakapowaeleza wanahabari.

    Mara ya kwanza kwa Rais Trump kuonekana kwenye kamera leo imeratibiwa saa 21:30 BST atakapotia saini tangazo linalohusiana na afya kutoka Ofisi ya Oval.

    Tukio hilo liko wazi kwa waandishi wa habari wa Ikulu ya White House leo, ikimaanisha kuwa waandishi wataweza kumuuliza maswali juu ya maswala mbali mbali, pamoja na operesheni ya Israeli.

  8. Habari za hivi punde, Netanyahu alikuwa katika makao makuu ya shirika la usalama la Israel wakati wa shambulio hilo

    .

    Chanzo cha picha, Shin Bet Media

    Shirika la usalama la Israel Shin Bet linasema Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alikuwa katika makao makuu ya idara hiyo wakati ujumbe wa Hamas uliposhambuliwa mjini Doha, Qatar.

    Shambulio hilo dhidi ya "uongozi mkuu" wa Hamas liliratibiwa kati ya shirika hilo na jeshi la Israel, msemaji wa Shin Bet anasema.

    Waziri wa ulinzi Israel Katz, naibu mkuu wa shirika la usalama na mkuu wa ujasusi wa kijeshi pia walikuwepo katika makao makuu, wanaongeza.

  9. Maswali mazito kuhusu shambulio la Israel Qatar

    Shambulio hili la Israel dhidi ya uongozi wa Hamas nchini Qatar ndilo ambalo wengi walihofia lingetokea, kutokana na dhamira ya baadhi ya serikali ya Israel kuendeleza kampeni ya "kulipa kisasi " kwa ajili ya uvamizi ulioongozwa na Hamas tarehe 7 Oktoba 2023 dhidi ya Israel.

    Ikionekana kupitia msukosuko huo, shambulio hili la Israel ni pigo la hivi punde zaidi la Israel dhidi ya maadui zake, iwe Gaza, Lebanon, Syria, Iran, Yemen na sasa Qatar.

    Pia inaweka kielelezo cha kutia wasiwasi kwa mazungumzo ya amani yajayo. Maswali kadhaa sasa yanahitaji majibu.

    Je, Marekani ilijua kuhusu shambulio hili mapema?

    Ikiwa ingejua yanakuja wakati huo, ikizingatiwa kuwa hili lilikuwa shambulio dhidi ya ardhi huru ya Qatar, hii itaathiri vipi kambi kubwa ya anga ya Marekani huko Qatar huko Al-Udeid?

    Je, itaathiri vipi uhusiano wa Marekani na washirika wake wote wa Ghuba ya Kiarabu?

    Ikiwa Qatar, ambayo ilikuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani ya Marekani na Taliban kabla ya 2021, si mahali salama, basi yatafanyika wapi?

  10. Iran yalaani shambulizi la Israel dhidi ya Qatar

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Esmail Baghaei alikuwa akizungumza kwenye TV ya serikali.

    Anasema hatua hiyo ilikuwa "ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa" na "ukiukaji wa uhuru wa kitaifa wa Qatar na wapatanishi wa Palestina".

    Ni lazima iwe kama "onyo zito kwa kanda na jumuiya ya kimataifa," msemaji wa wizara ya mambo ya nje anaongeza.

    Iran na Israel zimekuwa zikishikilia usitishaji mapigano tangu mwishoni mwa mwezi Juni.

  11. Israel yasema imewashambulia viongozi wakuu wa Hamas huku milipuko ikisikika huko Doha

    Moshi

    Chanzo cha picha, Reuters

    Milipuko imesikika na moshi umeonekana ukipanda juu ya mji mkuu wa Qatar Doha, shirika la habari la AFP na ripoti ya Reuters.

    Afisa wa Israel amethibitisha kuwa shambulizi hilo lililolenga viongozi wakuu wa Hamas lilifanyika nchini Qatar.

    Namna tukio hilo lilivyotokea bado haijawa wazi.

    Taarifa ilitolewa na jeshi la Israel ambalo linasema limefanya "shambulio sahihi" linalolenga viongozi wakuu wa Hamas.

    Taarifa hiyo haioneshi eneo la shambulizi. "Kabla ya shambulizi, hatua zilichukuliwa ili kupunguza madhara kwa raia, ikiwa ni pamoja na utumiaji wa risasi sahihi na ujasusi wa ziada," inaongeza taarifa hiyo.

    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Qatar amelaani "kwa maneno makali zaidi" shambulio ambalo Israel sasa imedai kuhusika.

    Dk Majed Al Ansari anasema shambulio hilo lilipiga majengo ya makazi "ambapo wanachama kadhaa wa ofisi ya kisiasa ya Hamas wanaishi katika mji mkuu wa Qatar, Doha".

    Anasema shambulio hilo linajumuisha "ukiukaji wa wazi" wa sheria za kimataifa na vile vile "tishio kubwa" kwa wale wa Qatar. "Nchi ya Qatar inalaani vikali shambulio hili, na inathibitisha kwamba haitavumilia tabia hii ya kizembe ya Israel na kuendelea kuhujumu usalama wa eneo hilo na hatua zozote zinazolenga usalama na mamlaka yake," inahitimisha taarifa hiyo.

    Unaweza kusoma;

  12. Harambee Stars yaicharaza bila jibu Ushelisheli

    Mshambuliaji matata wa timu ya taifa ya Harambee Stars Ryan Ogam alifunga mabao mawili na kuwatia moyo Harambee Stars kuongoza kwa mabao 4-0 dhidi ya Ushelisheli katika Mechi yao ya mwisho ya Kufuzu kwa Kombe la Dunia la FIFA 2026 katika Uwanja wa Kimataifa wa Michezo wa Moi, Kasarani Jumanne alasiri.

  13. Zaidi ya watu 20 waliuawa katika shambulio la Urusi huko Ukraine, Zelensky asema

    Zelensky

    Chanzo cha picha, Reuters

    Takribani watu 21 wameuawa katika shambulizi la anga la Urusi kwenye kijiji kimoja mashariki mwa Ukraine, wasema maafisa wa eneo hilo.

    Waathiriwa walikuwa watu wa kawaida wanaokusanya pensheni zao katika makazi ya Donetsk ya Yarova, alisema Rais Volodymr Zelensky.

    Kiongozi wa mkoa wa Donetsk Vadym Filkashkin alisema huduma za dharura zilikuwa katika eneo la tukio, na kwamba watu wengi walijeruhiwa.

    Yarova iko kaskazini mwa Sloviansk, moja ya miji mikubwa katika eneo hilo, na sio mbali na mstari wa mbele kwani vikosi vya Urusi vinasonga mbele polepole mashariki.

    Iwapo itathibitishwa, idadi ya vifo itakuwa miongoni mwa mashambulizi makali zaidi dhidi ya raia wa Ukraine katika wiki za hivi karibuni, miezi 42 baada ya uvamizi wa Urusi.

    Mwishoni mwa juma Urusi ilianzisha mashambulizi yake makubwa zaidi ya anga ya vita dhidi ya Kyiv hadi sasa, na kugonga jengo kuu la serikali katika mji mkuu, katika kile Zelensky alisema ni shambulio la "katili" lenye lengo la kurefusha vita.

    Akichapisha picha za picha za shambulio la Yarova mtandaoni, Zelensky alisema "hakuna maneno" ya kuelezea mashambulio ya hivi punde zaidi ya Urusi. Hakukuwa na majibu ya haraka kutoka kwa jeshi la Urusi.

    Unaweza kusoma;

  14. Zelensky: Putin anataka "kuichukua Donbass" ifikapo mwisho wa mwaka

    Zelensky

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Zelensky amesema Putin anataka "kuichukua Donbass" ifikapo mwisho wa mwaka, akisema itaigharimu Urusi maisha ya watu milioni mbili au tatu Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky aliiambia ABC TV kwamba Kremlin inataka "kuichukua Donbass" mwishoni mwa mwaka na kwamba rais wa Urusi "alizungumza juu ya hili na Wamarekani."

    "Yeye aliwaambia Wamarekani, Ikulu ya Marekani na mwakilishi wa Rais Trump Witkoff kwamba ataichukua Donbass baada ya miezi miwili au mitatu, ifikapo mwisho wa mwaka hivi karibuni, alisema ataichukua," Zelensky alimwambia mwandishi mkuu wa masuala ya kimataifa wa ABC News Martha Raddatz.

    Zelensky hakutaja chanzo chake cha habari hii. Vladimir Putin hajazungumza hadharani juu ya mipango ya Kremlin ya kuchukua Donbass hadi mwisho wa 2025.

    Mnamo Mei 2025, Bloomberg iliripoti, ikitoa mfano wa vyanzo, kwamba rais wa Urusi anaendelea na hali hii, jeshi la Urusi linachukua udhibiti kamili wa maeneo ya Donetsk, Luhansk, Kherson, Kherson, na mazungumzo mengine ya simu ya Ukraine.

    Akiwa na Rais wa Marekani Donald Trump. "Bei [ya kunyakua kwa Urusi sehemu ya eneo la Donetsk] ni miaka na watu milioni moja. Na ikiwa itatokea kwa kasi, basi kutakuwa na watu wengi zaidi, sio watu milioni, lakini maiti milioni mbili au tatu. Hiyo ndiyo bei yake," Zelensky aliongeza.

    Unaweza kusoma;

  15. Jeshi la Israel lawaamuru 'wakazi wote' wa Mji wa Gaza kuhama mara moja

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Jeshi la Israel linawaamuru "wakaazi wote" wa mji wa Gaza kuhama kabla ya mashambulizi mapya, baada ya Israel kuonya kuwa itaongeza mashambulizi yake ya kijeshi katika ukanda huo ikiwa Hamas haitawaachilia mateka wa mwisho inaowashikilia.

    Katika chapisho kwenye X, msemaji wa IDF wa lugha ya Kiarabu anasema kwamba itachukua hatua kwa "nguvu kubwa" katika Jiji la Gaza na kuwaonya wakaazi kuondoka.

    "Vikosi vya ulinzi vimedhamiria kuishinda Hamas na vitatenda kwa nguvu kubwa katika eneo la mji wa Gaza," Avichay Adraee amendika.

    Haya yanajiri baada ya baraza la mawaziri la usalama la Israel mwezi uliopita kuidhinisha mpango wa kuchukua udhibiti wa mji huo, ambapo mamia ya maelfu ya Wapalestina wanaishi.

    Ajith Sunghay, kutoka ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu (OHCHR), anaonya operesheni ya Israeli katika mji wa Gaza itakuwa "janga".

    "Tunachoenda kuona ni kitu ambacho hatujaona hapo awali ... wanaharibu kila kitu kinachohitajika kwa maisha ya raia," alikiambia kipindi cha BBC, BBC.Newsday

    "Miundo yote ya kiraia, iwe ni matanki ya maji, barabara, majengo, yote vimeharibiwa...tumeona katika sehemu ya kaskazini ya Gaza wameisawazisha, na tunahofia kuwa Jiji la Gaza litakabiliwa na matokeo sawa."

    Maelfu ya watu watakuwa wakijaribu kuhamia kusini, anasema, lakini asilimia fulani hawatahama.

    Wanajua wakiondoka hawataweza kurudi, ameongeza.

    Soma zaidi:

  16. ICC yafungua kesi ya uhalifu wa kivita dhidi ya kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Joseph Kony ameendesha uasi kwa zaidi ya miongo miwili

    Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu itafungua kesi dhidi ya mbabe wa kivita wa Uganda mtoro Joseph Kony, katika hatua ya kihistoria ya haki ya kimataifa karibu miongo miwili baada ya kutoa hati yake ya kwanza ya kukamatwa kwake.

    Siku ya Jumanne, majaji huko The Hague watachunguza makosa 39 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu dhidi ya Kony, ikiwa ni pamoja na mauaji, mateso, ubakaji, utumwa wa ngono na wizi.

    Kesi hiyo, inayojulikana kama uthibitisho wa kusikilizwa kwa mashtaka, itakuwa ya kwanza kuwahi kutokea kwa mahakama hiyo.

    Ingawa sheria za ICC zinakataza kusikilizwa kwa kesi kamili bila mshtakiwa kuwepo, waendesha mashitaka wanadai kuwa vikao ni muhimu ili kuhakikisha kesi inaweza kuendelea haraka iwapo Jospeph Kony hatimaye atakamatwa.

    Pia wanasema kwamba kupeleka madai yake ya uhalifu mbele ya mahakama ya kimataifa kunatoa kiwango cha utambuzi kwa waathiriwa, hata kama hayupo.

    Kony ambaye alikuwa mvulana wa madhabahuni Mkatoliki na baadaye kujiita nabii wa Lord's Resistance Army LRA amekwepa kukamatwa kwa miongo kadhaa.

    Uasi wake wa kikatili dhidi ya serikali ya Rais Yoweri Museveni ulisababisha vifo vya watu 100,000 na utekaji nyara wa watoto 60,000 kulingana na makadirio ya Umoja wa Mataifa.

    Unaweza pia kusoma:

  17. Putin amtunuku Jenerali Gerasimov, mwanajeshi mkuu wa Urusi, medali ya 'ujasiri'

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Urusi Vladimir Putin Jumatatu ametunukiwa Tuzo ya ujasiri kwa Jenerali wa Jeshi Valery Gerasimov, mkuu wa wafanyakazi wakuu wa vikosi vya jeshi la Urusi na kamanda mkuu wa vita vya Urusi nchini Ukraine.

    Gerasimov, mmoja wa watu wenye nguvu zaidi katika jeshi la Urusi na ambaye Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ilitoa waranti dhidi yake ya kukamatwa kwa madai ya uhalifu nchini Ukraine, anatajwa kuwa msanifu mkuu wa mkakati wa kisasa wa vita vya Urusi. Alitimiza umri wa miaka 70 Jumatatu.

    Gerasimov alipewa Tuzo ya ujasiri na mapambo ya kifahari ya serikali, "kwa ujasiri, ushujaa, na jitolea katika kutimiza wajibu wa kijeshi," kulingana na amri iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya sheria ya Urusi mwishoni mwa Jumatatu.

    Gerasimov anadhaniwa kushikilia mojawapo ya mikoba mitatu ya nyuklia inayoweza kutuma maagizo ya shambulio la nyuklia. Alitekeleza jukumu muhimu katika wakati Urusi ilipoitwaa Crimea kutoka kwa Ukraine mnamo 2014 na katika uungaji mkono wa kijeshi wa Urusi kwa Rais Bashar al-Assad katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Syria.

    Marekani ilimuwekea vikwazo siku moja baada ya uvamizi wa Urusi Februari 24, 2022 nchini Ukraine, ikisema alikuwa miongoni mwa waliohusika moja kwa moja. Putin alimteua Gerasimov kuongoza kampeni ya Ukraine mnamo Januari 2023.

  18. Wabunge wa Marekani watoa 'kitabu cha siku ya kuzaliwa' cha Epstein chenye madai ya saini ya Trump

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Epstein na Trump mnamo 1997 - wawili walikuw ana urafiki kwa miaka, lakini Trump anasema walitofautiana mapema katika miaka ya 2000.

    Wabunge wa Marekani wametoa nakala ya "kitabu cha siku ya kuzaliwa" alichopewa marehemu Jeffrey Epstein mfadhili wa watoto waliohukumiwa na hatia mwaka wa 2003, ambacho kinajumuisha barua inayodaiwa kutiwa saini na Rais wa Marekani Donald Trump.

    Kitabu hicho kilitolewa kikiwa na hati nyingi ambazo ni pamoja na wosia wa Epstein na kitabu chake cha anwani cha kibinafsi na mawasiliano ambayo yanajumuisha watu wa kifalme, watu mashuhuri, wanamitindo na wanasiasa kutoka kote ulimwenguni.

    Mawakili wa mali ya Epstein walituma hati kwa Kamati ya uangalizi ya bunge baada ya bunge kuwataka waiwasilishe.

    h

    Chanzo cha picha, X

    Maelezo ya picha, Wanademocrat kwenye Kamati ya Uangalizi ya Bunge walitoa picha hiyo Jumatatu, baada ya kamati hiyo kuipokea kutoka kwenye shamba la Epstein. Ikulu ya White House ilisema "Rais Trump hakuchora picha hii, na hakutia saini"

    Ikulu ya White House ilikanusha barua inayodaiwa kutoka kwa Trump, ambayo ilikuwa na mchoro wa mwili wa mwanamke, ilikuwa ya kweli na kusema rais "hakuchora picha hii, na hakusaini".

    Kitabu hicho chenye kurasa 238 kiliwekwa pamoja kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50 ya kuzaliwa kwa Epstein na Ghislaine Maxwell, mshiriki mwenzake wa Uingereza na mpenzi wake wa zamani ambaye alipatikana na hatia mwaka wa 2021 kwa kula njama naye kuwasafirisha wasichana kwa ajili ya ngono

    . Kiliandikwa mnamo 2003 - miaka mitatu kabla ya madai ya unyanyasaji wa kijinsia na Epstein kuwa hadharani.

    Kitabu hicho kilichochakaa, kilichoitwa "Miaka hamsini ya kwanza", kina mawasilisho, ambayo yanaonekana kutoka kwa watu mbalimbali marafiki wa Epstein, ikiwa ni pamoja na wanasiasa wa juu na viongozi wa biashara.

    Unaweza pia kusoma:

  19. Ufaransa katika mzozo mpya wa kisiasa baada ya wabunge kumtimua waziri mkuu

    g

    Chanzo cha picha, AFP Via Getty

    Maelezo ya picha, Waziri Mkuu François Bayrou

    Ufaransa imetumbukia katika mzozo mpya wa kisiasa baada ya kushindwa kwa Waziri Mkuu François Bayrou katika kura ya imani katika Bunge la taifa.

    Kushindwa kwa Bayrou kwa kura 364 dhidi ya 194 kunamaanisha kwamba Jumanne atawasilisha barua ya kujiuzulu kwa serikali yake kwa Rais Emmanuel Macron, ambaye lazima sasa aamue kuhusu hatua zitakazofuata. Ofisi ya Macron ilisema hii itafanyika "katika siku zijazo".

    Hatua zitakazochukuliwa na kumtaja waziri mkuu mpya kutoka mrengo wa kulia wa kati; kuelekea kushoto na kutafuta jina linaloendana na Chama cha Kisoshalisti; na kuvunja bunge ili uchaguzi mpya ufanyike.

    Bayrou amekuwa waziri mkuu wa kwanza katika historia ya Ufaransa ya miaka ya karibuni kuondolewa madarakani kwa kura ya imani badala ya kura ya kutokuwa na imani naye.

    Ofisi ya rais wa Ufaransa ilisema katika taarifa yake kwamba rais Emmanuel Macron "amezingatia" matokeo na kusema atamtaja waziri mkuu mpya "katika siku zijazo", na kufikisha mwisho uvumi uliobaki kwamba rais badala yake anaweza kuitisha uchaguzi wa mapema.

    Macron atakutana na Bayrou Jumanne "kukubali kujiuzulu kwa serikali yake", iliongeza.

    Bayrou ni waziri mkuu wa sita chini ya Macron tangu kuchaguliwa kwake mnamo mwaka 2017 lakini wa tano tangu 2022. Kuondolewa kwa Bayrou kunamwacha mkuu huyo wa taifa la Ufaransa na mtihani mpya wa ndani ya nchi unaomumiza kichwa katika wakati anapoongoza juhudi za kidiplomasia kuhusu vita vya Urusi dhidi ya Ukraine.

    Maadui wakubwa wa Macron katika chama cha mrengo wa kushoto cha France Unbowed wanamtaka yeye binafsi kujiuzulu, lakini wachambuzi wachache wanafikiri hilo linawezekana.

    Kwa hivyo Ufaransa iko njiani kupata waziri mkuu wa tano katika kipindi cha chini ya miaka miwili, rekodi mbaya ambayo inadhihirisha kuyumba na kutoridhika ambako kumetawala katika muhula wa pili wa rais nchini Ufaransa.

  20. Israel yafanya uvamizi viungani mwa miji ya na Homs na Latakia nchini Syria

    h

    Chanzo cha picha, SANA

    Israel imeanzisha mashambulizi ya anga Jumatatu jioni viungani mwa miji ya Homs na Latakia, nchini Syria, rasmi za vyombo vya habari vya Syria zimesema.

    Uvamizi wa Israel ulilenga eneo la Maskana viungani mwa Homs.

    Mashambulizi kama hayo ya ndege pia yalilenga maeneo ya karibu na eneo la Saqoubin nje kidogo ya Latakia, lakini hakuna hasara iliyoripotiwa, kulingana na shirika la habari la Syria, ambalo lilithibitisha kuwa magari ya zima moto yalitumwa kwenye eneo la shambulio hilo.

    Kwa upande wake, Shirika la uangalizi wa haki za inadamu la Syria limeripoti kuwa "ndege za kivita za Israel zilifanya shambulizi la anga zikilenga kikosi cha anga kilichoko kusini mashariki mwa mji wa Homs. Milipuko mikubwa ilisikika katika eneo lililolengwa, huku kukiwa na ripoti za awali za uharibifu wa mali."

    Wizara ya mambo ya nje ya Syria ililaani "uvamizi wa anga unaofanywa na vikosi vya Israel vinavyokalia kwa mabavu," kama ilivyoeleza, na kuyataka kama "ukiukaji wa wazi" wa sheria za kimataifa na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa.

    Ilisema kuwa uvamizi huu "ni sehemu ya mfululizo wa mashambulizi ya uchokozi yanayofanywa na Israeli kwenye ardhi ya Syria''.

    Unaweza pia kusoma: