'Sio vita vyetu' - Mkataba wa Trump wa silaha za Nato kwa Ukraine waibua hasira za MAGA

Baadhi ya wanachama wa kihafidhina wa vuguvugu la Donald Trump la "Make America Great Again" wamejibu kwa hasira mipango ya rais ya kuiuzia Nato silaha, wakisema ni usaliti wa ahadi yake ya kukomesha ushiriki wa Marekani katika vita vya kigeni.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Dinah Gahamanyi na Abdalla Seif Dzungu

  1. Lamine Yamal mashakani kuhusiana na mzozo wa walemavu

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Lamine yamal

    Wizara ya Haki za Kijamii ya Uhispania imeitaka ofisi ya mwendesha mashtaka wa nchi hiyo kumchunguza winga wa Barcelona Lamine Yamal baada ya kuripotiwa kuwaajiri watu wenye ulemavu kutumbuiza kwenye sherehe yake ya kutimiza miaka 18.

    Lamine Yamal aliandaa karamu siku ya Jumapili katika nyumba iliyokodishwa huko Olivella, mji mdogo ulio kilomita 50 kaskazini magharibi mwa Barcelona, na wageni wakiwemo WanaYouTube, washawishi, na wachezaji wenzake kadhaa wa Barcelona.

    Inadaiwa Lamine Yamal alikodisha kikundi cha watumbuizaji walio na ulemavu, jambo ambalo Chama cha Watu wenye Achondroplasia na Dysplasias nyingine za Mifupa nchini Uhispania (ADEE) kilieleza kuwa "halikubaliki katika karne ya 21".

    Ilipowasiliana na BBC Sport, Kurugenzi Kuu ya Watu Wenye Ulemavu - sehemu ya Wizara ya Haki za Kijamii, Masuala ya Watumiaji, na Agenda ya 2030 - ilisema: "ADEE imewasilisha malalamiko ya kisheria.

    “Kwa hiyo, Kurugenzi Kuu imeitaka Ofisi ya Mwendesha Mashtaka kufanya uchunguzi ili kubaini iwapo sheria na hivyo haki za watu wenye ulemavu zimekiukwa.

    ADEE ilisema "inashutumu hadharani uajiri wa watu wenye ulemavu wa ngozi kama sehemu ya burudani," na ikasema itachukua hatua za kisheria kwani "inaendeleza dhana potofu, inachochea ubaguzi, na inadhoofisha taswira na haki" za watu wenye ulemavu.

    Katika taarifa ilisema: "Vitendo hivi vinakiuka sio tu sheria za sasa lakini pia maadili ya kimsingi ya jamii inayotaka kuwa na usawa na heshima.

    "Sheria ya jumla juu ya haki za watu wenye ulemavu inakataza kwa uwazi vitendo vifuatavyo: 'Maonyesho au shughuli za burudani ambazo watu wenye ulemavu au hali zingine hutumiwa kuchochea dhihaka, au kejeli kutoka kwa umma kwa njia inayopingana na heshima inayostahili utu ni marufuku'."

    Hata hivyo, kituo cha redio cha Uhispania RAC1, external kilitangaza mahojiano na mtu aliyedai kuwa mmoja wa waburudishaji waliokuwepo kwenye tafrija hiyo ambaye alimtetea Lamine Yamal.

    “Hakuna aliyetudharau, tulifanya kazi kwa amani,” alisema msanii huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina. "Sielewi kwa nini kuna hype nyingi. Sisi ni watu wa kawaida, ambao hufanya tunachotaka, kwa njia ya kisheria kabisa. "Tunafanya kazi kama watumbuizaji. Kwa nini hatuwezi kufanya hivyo? Kwa sababu ya hali yetu ya kimwili? "Tunajua kikomo chetu ni nini na hatutawahi kuvuka: sisi sio nyani."

    Mwigizaji huyo alisema ilichukua saa moja, na baadaye watumbuizaji wakajiunga na tafrija hiyo.

    "Tunacheza, tunasambaza vinywaji, tunafanya uchawi ... kuna aina nyingi za maonyesho. Kila mtu alikuwa na wakati mzuri."

  2. Maelfu ya Waafghanistan walihamia Uingereza kwa mpango wa siri

    Askari

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelfu ya Waafghanistan wamehamishwa hadi Uingereza chini ya mpango wa siri ambao ulianzishwa baada ya afisa wa Uingereza kuvujisha data zao bila kukusudia, inaweza kufichuliwa.

    Mnamo Februari 2022, maelezo ya binafsi ya karibu watu 19,000 ambao walikuwa wametuma maombi ya kuhamia Uingereza baada ya Taliban kunyakua mamlaka nchini Afghanistan yalipotea.

    Serikali ya awali ilipata habari kuhusu ukiukaji huo mnamo Agosti 2023 na ikaunda mpango mpya wa makazi mapya miezi tisa baadaye.

    Imeshuhudia Waafghani 4,500 wakiwasili Uingereza, na watu zaidi ya 600 na familia zao za karibu bado kuwasili.

    Kuwepo kwa mpango wa uvujaji na uhamishaji ulifanyika siri kwa zaidi ya miaka mitatu baada ya serikali kupata amri ya juu.

    Maelezo ya ukiukaji mkubwa wa data, mwitikio na idadi ya Waafghanistan waliopewa haki ya kuishi nchini Uingereza kutokana na hilo yaliwekwa wazi siku ya Jumanne baada ya jaji wa Mahakama Kuu kutoa uamuzi kwamba agizo la kufungwa linapaswa kuondolewa.

    Uvujaji huo ulikuwa na majina, maelezo ya mawasiliano na baadhi ya taarifa za kifamilia za watu ambao wanaweza kuwa katika hatari ya madhara kutoka kwa Taliban.

    Akizungumza katika Baraza la Commons, Waziri wa Ulinzi John Healey alitoa "msamaha wa dhati" kwa wale ambao maelezo yao yalikuwa yamejumuishwa katika uvujaji huo, ambao ulikuja kujulikana wakati baadhi ya maelezo yalipoonekana kwenye Facebook.

    Alisema ilikuwa ni matokeo ya orodha kutumwa kwa barua pepe "nje ya mifumo ya serikali iliyoidhinishwa", ambayo alielezea kama "kosa kubwa la idara" , ingawa Polisi wa Metropolitan tayari wameamua uchunguzi wa polisi haukuwa muhimu.

    Healey alisema uvujaji huo ni "moja ya hasara nyingi za data" zinazohusiana na uhamishaji wa Afghanistan katika kipindi hicho, na ilikuwa na majina ya maafisa wakuu wa jeshi, maafisa wa serikali, na wabunge.

    Unaweza kusoma;

  3. 'Sio vita vyetu' - Mkataba wa Trump wa silaha za Nato kwa Ukraine waibua hasira za MAGA

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Marjorie Taylor Greene alisema alipinga "mkataba wa nyuma kupitia Nato" wa kuipatia Ukraine silaha

    Baadhi ya wanachama wa kihafidhina wa vuguvugu la Donald Trump la "Make America Great Again" wamejibu kwa hasira mipango ya rais ya kuiuzia Nato silaha, wakisema ni usaliti wa ahadi yake ya kukomesha ushiriki wa Marekani katika vita vya kigeni.

    Siku ya Jumatatu, Trump alisema atatuma silaha kwa Ukraine kupitia Nato, huku pia akitishia Urusi kwa kutoza ushuru zaidi ikiwa makubaliano ya kumaliza vita hayatafikiwa ndani ya siku 50.

    Wabunge wa chama cha Republican, Marjorie Taylor Greene, mshirika mkuu wa Trump, na mwanamikakati wa zamani wa Trump Steve Bannon ni miongoni mwa waliokosoa uamuzi huo, huku Bannon akiwaambia wasikilizaji wake wa podikasti kwamba Ukraine ni "vita vya Ulaya".

    Ikulu ya White House imesisitiza kuwa Ulaya itagharamia silaha hizo zinazotengenezwa na Marekani.

    Katika mahojiano na gazeti la New York Times, Greene - mwanachama aliyejitenga na Bunge kutoka Georgia ambaye amekuwa mmoja wa wafuasi waaminifu zaidi wa Trump huko Capitol Hill - alisema hatua hiyo inakinzana na kile alichowaahidi wapiga kura kwenye kampeni.

    "Siyo Ukraine pekee; yote ni vita vya nje kwa ujumla na misaada mingi kutoka nje," alisema. "Hili ndilo tulilofanya kampeni. Hili ndilo nililoahidi pia kwa wilaya yangu. Hili ndilo ambalo kila mtu alilipigia kura. Na ninaamini kwamba tunapaswa kudumisha barabara hiyo."

  4. Wanaharakati wa Sudan: Vikosi vya RSF viliwaua watu 300 katika jimbo la Kordofan Kaskazini

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Wapiganaji wa RSF

    Wanaharakati wa Sudan walisema Jumatatu kwamba Vikosi vya RSF viliwaua karibu watu 300 katika mashambulizi katika jimbo la Kordofan Kaskazini yaliyoanza Jumamosi.

    Vikosi vya RSF vinashiriki katika vita dhidi ya jeshi la Sudan katika eneo hili, ambalo limekuwa moja ya pande kuu katika mzozo ambao umekuwa ukiendelea tangu Aprili 2023.

    Jeshi limechukua udhibiti wa maeneo ya kati na mashariki mwa nchi, wakati Vikosi vya RSF vikijitahidi kuimarisha udhibiti wao katika mikoa ya magharibi, ikiwa ni pamoja na Kordonfan Kaskazini.

    Shirika la Wanasheria wa Dharura wa Haki za Kibinadamu lilisema katika taarifa siku ya Jumatatu kwamba Vikosi vya (RSF) vilishambulia vijiji kadhaa siku ya Jumamosi karibu na mji wa Bara inaoudhibiti.

    Aliliambia shirika la kutetea haki za binadamu, ambalo linaandika ukatili wa vita vya miaka miwili kati ya jeshi na Rapid Support Forces, kwamba raia waliuawa kwa wingi siku ya Jumapili wakati wanajeshi wa RSF walipovamia kijiji cha Umm Qirfa katika jimbo la Kordofan Kaskazini, ambapo pia waliharibu nyumba na kupora mali.

    Shirika hilo pia limeongeza kuwa katika kijiji cha Shaq al-Num, zaidi ya watu 200 walichomwa moto hadi kufa au kupigwa risasi.

    Unaweza kusoma;

  5. Ufaransa: Bila makubaliano ya nyuklia na Iran, tutaanza kurejesha vikwazo dhidi yake ndani ya mwezi mmoja na nusu

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa anajadili matumizi ya mfumo wa vichochezi kabla ya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noël Barrow amesema iwapo hakuna maendeleo madhubuti yatapigwa katika makubaliano ya nyuklia na Iran, nchi tatu za Ufaransa, Uingereza, na Ujerumani zitaanzisha utaratibu wa kurejesha moja kwa moja vikwazo vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran ifikapo mwishoni mwa Agosti, ambayo ni takriban wiki sita kabla.

    "Ufaransa na washirika wake wana haki ya kuweka tena vikwazo vya kimataifa [dhidi ya Iran] kwa silaha, benki na vifaa vya nyuklia ambavyo viliondolewa miaka 10 iliyopita," aliwaambia waandishi wa habari.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa alisema: "Bila ya dhamira thabiti, inayoonekana na inayoweza kuthibitishwa na Iran, tutachukua hatua hii mwishoni mwa Agosti hivi karibuni."

    Bwana Barrow ametangaza hayo leo, kabla ya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels.

    Esmail Baghaei, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, alisema jana kuhusu uanzishaji wa utaratibu huo: "Kile ambacho kimeitwa mfumo wa snapback hakina msingi wa kisheria au wa kisiasa. Sasa, kwa kuzingatia hatua zilizopigwa, kutumia utaratibu kama huo kunazidi kutokuwa na msingi wa kisheria na wa kimaadili. Inasaidia tu uwezekano ambao ulijumuishwa katika Azimio33 na ufafanuzi 22."

    Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi, ambaye alisafiri hadi China kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai, alikutana na mawaziri wenzake wa China na Urusi.

    Nchi hizi mbili ambazo ni wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zinapinga kurejeshwa kwa vikwazo dhidi ya Iran.

    Unaweza kusoma;

  6. 'Sijuti kufanya maamuzi magumu kwa Kenya' - Ruto

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais William Ruto

    Rais William Ruto amepuuzilia mbali wapinzani wake wa kisiasa akisisitiza kujitolea kwake kupunguza gharama ya maisha na kuimarisha usalama wa chakula.

    Akithibitisha kujitolea kwake kuleta utulivu wa uchumi, Ruto Jumanne alisema kuwa ukosoaji kutoka kwa baadhi ya maeneo hautamzuia kutekeleza mpango wake.

    "Tuna mpango wa jinsi ya kutengeneza nafasi za kazi marafiki zangu. Kwa hivyo mtu asiwadanganye. Unajua unaposikia watu wakizungumza ni kana kwamba Kenya ndiyo nchi mbaya zaidi duniani," alisema kiongozi wa taifa.

    Ruto aliongeza kuwa sio nchi nyingi zinaweza kufikia kile ambacho Kenya imefanikisha muda kwa muda mfupi.

    "Lazima tuwakatae wale wanaotaka kutuambia vinginevyo ... kwamba oh, wewe Kenya ni nchi iliyoshindwa. Je! unajua nchi iliyoparaganyika inaonekanaje?" aliuliza.

    Ruto alisisitiza kuwa ajenda yake kwa nchi bado haiwezi kubadilishwa na takwimu kuhusu hali ya uchumi zinathibitisha kuwa yuko sahihi.

    "Unaweza kusema chochote unachotaka kusema. Nimelazimika kufanya maamuzi magumu sana ili kutufikisha hapa na sijutii hata kidogo," Ruto aliongeza.

    Aliongeza kuwa serikali ina nia ya kuhakikisha uchumi unakuwa katika hali ya juu.

    Unaweza kusoma;

  7. 'Trump alimuuliza Zelensky iwapo anaweza kushambulia mjini Moscow' - Financial Times

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Trump na Zelensky

    Gazeti la Uingereza la Financial Times linathibitisha kuwa Rais wa Marekani Donald Trump hivi majuzi alimuuliza Volodymyr Zelensky iwapo Ukraine inaweza kushambulia Moscow na St. Petersburg.

    Wa kwanza kuripoti juu ya mazungumzo kama haya alikuwa mwandishi wa gazeti la Washington Post David Ignatius, akimnukuu mpatanishi wake katika Ikulu ya White House, ambaye alikuwa akifahamu yaliyomo kwenye simu ya hivi karibuni kati ya Trump na Zelensky.

    Vyanzo viwili vya Financial Times pia viliripoti kwamba Trump alimuuliza Zelensky "kama angeweza kulenga shabaha za kijeshi ndani ya Urusi ikiwa atapata silaha zenye uwezo huo." "Vladimir, unaweza kushambulia Moscow? Unaweza kupiga St Petersburg pia?" Trump aliuliza, kulingana na vyanzo vya FT.

    Kwa mujibu wa taarifa zao, Zelensky alijibu: "Kabisa. Tunaweza, ikiwa unatupa silaha." Vyanzo vya mwandishi wa Washington Post pia viliripoti kuwa utawala wa Trump unazingatia uwezekano wa kuipatia Ukraine makombora ya masafa ya kati ya Tomahawk ya Marekani.

    Nakala ya FT kuhusu suala hilo inasema: "Waukraine walikuwa wameomba Tomahawks, makombora ya kuongozwa kwa usahihi yenye masafa ya takriban kilomita 1,600.

    Lakini utawala wa Trump - kama utawala wa Biden - ulikuwa na wasiwasi juu ya ukosefu wa kujizuia kwa Ukraine, kulingana na mtu anayefahamu orodha [ya silaha za Marekani zinazotolewa kwa Ukraine] ambayo ilionyeshwa kwa Zelensky."

    Watu wanaofahamu mazungumzo kati ya Trump na Zelensky pia waliambia FT kwamba Trump alikusudia kuwafanya Warusi "kuhisi uchungu" na hivyo kuwalazimisha kujadili.

    Kwa mujibu wa afisa mmoja wa nchi za Magharibi ambaye hakutajwa jina aliyetajwa na waandishi wa chapisho hilo, mazungumzo kati ya marais wa Ukraine na Marekani yanaonyesha hamu inayoongezeka ya washirika wa Kyiv kuwapatia Wanajeshi wa Ukraine silaha za masafa marefu zenye uwezo wa "kupeleka vita Moscow."

    Unaweza kusoma;

  8. Mchekeshaji maarufu Kenya anayemuiga aliyekuwa Naibu wa Rais Kenya aaga dunia

    .

    Chanzo cha picha, Kafengo Facebook

    Maelezo ya picha, KK Mwenyewe maarufu Riggy G

    Mcheshi maarufu wa Kenya KK Mwenyewe, anayejulikana sana kwa uigaji wake wa mtandaoni wa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

    KK, jina halisi Zachariah Kariuki, alitangazwa kufariki Jumatatu usiku katika Hospitali ya Kiambu Level 4, kulingana na mcheshi mwenzake na mshiriki wa mara kwa mara, Kafengo.

    Katika ujumbe wake mzito, Kafengo alisema, “Pumzika kwa amani kaka, utabaki mioyoni mwetu milele, kwa familia na marafiki, Mungu atupe nguvu katika kipindi hiki kigumu.

    KK Mwenyewe alijipatia umaarufu mkubwa kwenye mitandao ya kijamii mwishoni mwa 2022 kwa ucheshi wake na kejeli za kisiasa, mara nyingi akiiga mtindo na tabia za kipekee za Gachagua mara nyingi kwa usahihi kabisa.

    Maelezo kuhusu ugonjwa wake na matukio ya mwisho bado yanajitokeza, lakini sifa zinaendelea kumiminika huku watu wakikumbuka ucheshi wake usio na kifani .

    Mchekeshaji huyo mchanga, alipata umaarufu mara tu baada ya serikali ya Kenya Kwanza kuchukua mamlaka, aliona umaarufu wake ukizidi kuzua matumaini ya umma kwamba aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua angetambua na kuunga mkono talanta yake kama alivyofanya kwa Ivy Chelimo, mwanadada aliyebuni jina la utani 'Riggy G'.

    .

    Chanzo cha picha, Kafengo facebook

    Maelezo ya picha, KK Mwenyewe akimuiga aliyekuwa naibu wa rais wa Kenya Rigathi Gachagua
  9. Rais wa zamani wa Nigeria Buhari kuzikwa nyumbani kwake

    Muhammadu Buhari

    Chanzo cha picha, Pius Utomi Ekpei/ Getty images

    Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari atazikwa katika uwanja wa nyumba yake katika jimbo la kaskazini la Katsina siku ya Jumanne, Gavana wa jimbo hilo Dikko Radda aliambia BBC Hausa.

    Radda alikuwa na familia ya Buhari mjini London, ambako alifariki katika kliniki siku ya Jumapili akiwa na umri wa miaka 82.

    Mwili wa Buhari uliondoka London Jumanne asubuhi kwa ndege ya rais wa Nigeria.

    Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na gavana wa Katsina, mwili wa rais huyo wa zamani utasafirishwa moja kwa moja hadi jimboni kwake kabla ya kuhamishiwa katika makazi yao ya mwisho katika mji wa Daura anakozaliwa Buhari, maili 50 (kilomita 80) kutoka mji wa Katsina.

    Nyumba ya Buhari tayari imejaa waombolezaji huku marafiki, familia na watu wenye mapenzi mema wakisubiri kuwasili kwa maiti yake ambayo itatarajiwa baada ya saa sita mchana (11:00 GMT).

    Serikali ya Nigeria ilikuwa imetangaza Jumanne kuwa siku ya mapumziko kwa ajili ya kumuenzi Buhari ambaye pia alikuwa jenerali wa zamani wa jeshi, mmoja wa Wanigeria wawili pekee walioongoza nchi hiyo kama kiongozi wa kijeshi na rais aliyechaguliwa kidemokrasia.

    Waziri wa Habari wa Nigeria Mohammed Idris hapo awali alitangaza kuwa shughuli ya kijeshi na sala ya Kiislamu itafanyika kwa ajili ya Buhari huko Daura.

    Maafisa wanasema mazishi, ambayo yalitarajiwa hapo awali Jumatatu, yalicheleweshwa kwa sababu za taratibu za mipango.

    Unaweza kusoma;

  10. Watu 15 wakamatwa Uganda kwa kuharibu mabango ya kampeni ya rais

    Yoweri Museveni ni mmoja wa marais waliokaa madarakani muda mrefu barani Afrika

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Yoweri Museveni ni mmoja wa marais waliokaa madarakani muda mrefu barani Afrika

    Wanachama 15 wa chama cha upinzani cha National Unity Platform nchini Uganda, wameshtakiwa kwa kuharibu mabango ya kampeni ya Rais Yoweri Museveni, kwa mujibu wa ripoti ya tovuti ya kibinafsi ya Chimp.

    Polisi wanasema 15 hao waliharibu mabango katika mji mkuu wa Kampala siku chache kabla ya ziara rais katika eneo hilo.

    "Washukiwa wanashtakiwa chini ya Kifungu cha 78(2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Urais, ambayo inaharamisha upotoshaji wa matangazo na nyenzo za kampeni," Chimp Reports alisema.

    Washukiwa hao wanazuiliwa katika gereza la Luzira na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 29 Julai.

    Kukamatwa kwa watu hao kunakuja huku joto la kisiasa likipanda baada ya Museveni kuteuliwa tarehe 5 Julai kama mgombea wa chama tawala cha National Resistance Movement katika uchaguzi wa rais wa Januari ujao.

    Iwapo atachaguliwa tena, Museveni, 80, ambaye aliingia mamlaka mwaka 1986, anaweza kuendeleza utawala wake hadi takriban miaka 50.

    Maelezo zaidi:

  11. Vikosi vya Ethiopia 'viliwauwa' wafanyakazi wa misaada Tigray, shirika la misaada lasema

    g

    Chanzo cha picha, MSF

    Maelezo ya picha, Watatu hao walisemekana kuwa weledi na wapenda kazi zao

    Vikosi vya serikali ya Ethiopia "vimewaua" wafanyakazi watatu wa shirika la kutoa misaada la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF) walipokuwa kwenye misheni ya kibinadamu katika eneo lililokumbwa na vita la Tigray kaskazini mwa Ethiopia miaka minne iliyopita, afisa mkuu wa MSF ameiambia BBC.

    Raquel Ayora ameyasema hayo wakati MSF ilipokuwa ikitoa matokeo yake katika kile ilichokiita mauaji ya "kusudi na yaliyolenga" ya watatu hao - raia wa Uhispania na Waethiopia wawili - katika kilele cha mzozo uliomalizika wa Tigray.

    "Walinyongwa," alisema Bi Ayora, mkurugenzi mkuu wa MSF Uhispania. "Walikuwa wakikabiliana na washambuliaji wao [na] walipigwa risasi karibu sana... mara kadhaa."

    BBC imeiomba serikali ya Ethiopia kujibu tuhuma hizo.

    MSF ilisema inatoa matokeo yake kwani serikali imeshindwa kutoa "hesabu ya kuaminika" ya vifo hivyo licha ya mikutano 20 ya ana kwa ana katika kipindi cha miaka minne iliyopita.

    Mhispania María Hernández Matas mwenye umri wa miaka thelathini na mitano, pamoja na Yohannes Halefom Reda mwenye umri wa miaka 32 na Tedros Gebremariam mwenye umri wa miaka 31, waliuawa tarehe 24 Juni 2021 walipokuwa wakisafiri katikati mwa Tigray kutathmini mahitaji ya matibabu.

    "Walikuwa wataalamu sana na wenye shauku," Bi Ayora aliiambia BBC.

  12. Meta kutumia mamia ya mabilioni kujenga vituo vya data vya Akili Mnemba

    h

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mwanzilishi wa Meta Mark Zuckerberg amesema kampuni kubwa ya mitandao ya kijamii itatumia mamia ya mabilioni ya dola kujenga vituo vikubwa vya data vya Akili Mnemba (AI) nchini Marekani.

    Kituo cha kwanza cha data cha gigawati nyingi, kiitwacho Prometheus, kinatarajiwa kuanza kufanya kazi mnamo mwaka 2026, Zuckerberg anasema.

    Alisema moja ya tovuti itashughulikia eneo lenye ukubwa wa karibu sawa na jiji la Manhattan (59.1 kilomita za mraba).

    Meta imewekeza sana katika juhudi za kukuza kile ilichokiita "ujasusi mkubwa" - teknolojia ambayo ilisema inaweza kuwawazidi wanadamu wenye akili zaidi.

    Kampuni hiyo, ambayo imepata pesa zake nyingi kutokana na utangazaji wa mtandaoni, ilizalisha mapato ya zaidi ya $160bn mwaka wa 2024.

    Katika chapisho kwenye jukwaa lake la mitandao ya kijamii, Threads, Zuckerberg alisema Meta ilikuwa ikiunda makundi kadhaa ya gigawati nyingi, na kwamba nguzo moja, inayoitwa Hyperion, inaweza kuongeza hadi gigawati tano kwa miaka kadhaa.

    "Tunaunda makundi mengi zaidi ya titan pia. Moja tu ya hizi inashughulikia sehemu za Manhattan," aliongeza.

    Prometheus itajengwa katika majimbo ya New Albany, Ohio, wakati Hyperion itajengwa Louisiana na inatarajiwa kuwa mtandaoni kikamilifu ifikapo 2030, Zuckerberg alisema.

    Alisema Meta "itawekeza mamia ya mabilioni ya dola... kujenga ujasusi mkubwa" na kwamba vituo vilikuwa vimepewa "majina yanayolingana na ukubwa na athari zake".

    Karl Freund, mchambuzi mkuu katika Utafiti wa Aliki Mnemba wa Cambrian, aliiambia BBC, "ni wazi, Zuckerberg anakusudia kutumia njia yake ya Akili Mnemba".

  13. Nimesikitika lakini sijakata tamaa na Putin, Trump aiambia BBC

    h

    Chanzo cha picha, Reuters

    Donald Trump amesema amesikitishwa na Putin lakini akasema bado hajakata tamaa na Vladimir Putin, katika mazungumzo ya kipekee ya simu na BBC.

    Rais wa Marekani alishinikizwa iwapo anamuamini kiongozi huyo wa Urusi, na akajibu: "Sina imani na mtu yeyote."

    Trump alikuwa akizungumza saa chache baada ya kutangaza mipango ya kutuma silaha kwa Ukraine na kuonya kuhusu ushuru mkali kwa Urusi ikiwa hakutakuwa na makubaliano ya kusitisha mapigano ndani ya siku 50.

    Katika mahojiano marefu kutoka kwa Ofisi yake ya Oval, rais pia aliidhinisha Nato, baada ya mara moja kuielezea kama iliyopitwa na wakati, na kuthibitisha kuunga mkono kanuni ya ulinzi ya pamoja ya shirika hilo.

    Rais Trump aliipigia simu BBC katika mazungumzo yaliyodumu kwa muda wa dakika 20, baada ya mazungumzo kuhusu mahojiano yanayoweza kuadhimisha mwaka mmoja tangu jaribio dhidi ya maisha yake lilipotokea katika mkutano wa kampeni huko Butler, Pennsylvania.

    Alipoulizwa iwapo kunusurika kwenye jaribio la mauaji kumembadilisha, Trump alisema alipenda kulifikiria kidogo iwezekanavyo kuhusu hilo.

    "Sipendi kufikiria ikiwa ilinibadilisha," Trump alisema. Kufikiria kulihusu, "inaweza kubadilisha maisha".

    Baada tu ya kukutana na mkuu wa Nato Mark Rutte katika Ikulu ya White House, hata hivyo, rais alitumia sehemu kubwa ya mahojiano kuelezea kwa mapana kuhsuu kukatishwa tamaa kwake na kiongozi wa Urusi.

    Trump alisema kuwa alifikiri kwamba makubaliano yalikuwa kwenye yamefikiwa na Urusi mara nne tofauti.

    Unaweza pia kusoma:

  14. Wanyama huguswa na sauti za siri kutoka kwa mimea, wasema wanasayansi

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wanyama huguswa na sauti zinazofanywa na mimea, utafiti mpya unapendekeza, na kufungua uwezekano kwamba mfumo wa ikolojia usioonekana unaweza kuwepo kati yao.

    Katika ushahidi wa kwanza kama huo, timu katika Chuo Kikuu cha Tel Aviv iligundua kuwa nondo wa kike waliepuka kuweka mayai yao kwenye mimea ya nyanya kama ingetoa kelle walizohusisha na dhiki, ikionyesha kuwa wanaweza kuwa na afya mbaya.

    Timu hiyo ya wanasayansi ilikuwa ya kwanza kuonyesha miaka miwili iliyopita kwamba mimea hupiga kelele ikiwa imefadhaika au inapokuwa katika hali mbaya.

    Sauti hizo ziko nje ya masafa ya usikivu wa binadamu, lakini zinaweza kutambuliwa na wadudu wengi, popo na baadhi ya mamalia.

    "Hili ni onyesho la kwanza la mnyama anayeitikia sauti zinazotolewa na mmea," Prof Yossi Yovel wa Chuo Kikuu cha Tel Aviv alisema.

    "Hizi ni tetesi tu katika hatua hii, lakini inaweza kuwa kwamba aina zote za wanyama watafanya maamuzi kulingana na sauti wanazosikia kutoka kwa mimea, wakati wa kuchavusha au kujificha ndani yake au kula mmea."

    Watafiti walifanya mfululizo wa majaribio yaliyodhibitiwa kwa uangalifu ili kuhakikisha kuwa nondo zinaitikia sauti na sio kuonekana kwa mimea.

    Sasa watachunguza sauti ambazo mimea tofauti huzitoa na ikiwa spishi zingine hufanya maamuzi kulingana na sauti hizo, kama vile kuchavusha au kujificha ndani yake au kula mmea.

  15. Umri wa kunywa pombe kuongezwa Kenya hadi miaka 21

    g

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mamlaka ya Kitaifa ya Kampeni dhidi ya matumizi mabaya ya pombe na dawa za kulevya (NACADA) inapanga kutekeleza sheria kali zaidi kuhusu uuzaji na unywaji wa pombe na dawa za kulevya.

    Sera ya taifa hilo ya kudhibiti matumizi haramu ya pombe, na dawa za kulevya yam waka 2025 inapendekeza hatua kali ambazo Mamlaka inaamini zitamaliza tatizo la unywaji pombe uliokubuhu nchini, haususan miongoni mwa vijana.

    Baadhi ya sheria hizo ni pamoja na kupiga marufuku uuzwaji wa pombe karibu na shule na maeneo ya ibada, huku ikisisitizia marufuku ya unyanyasaji wa pombe wa kupindukia na matumizi ya madawa ya kulevya.

    Kadhalika, sera hiyo inalenga kuzuia uuzaji wa pombe kwa watoto walio chini ya chini ya miaka 21 huku pia ikiimarisha ulinzi kwa wale wanaotaka kujiepusha na pombe na dawa za kulevya.

    Baraza la Mawaziri liliidhinisha sera hiyo mnamo mwezi wa Juni 24, baada ya serikali ikuiruhusu mamlaka hiyo kutekeleza sheria mpya.

    Takwimu ziliripoti kuwa asilimia 87.3 ya wanafunzi hutumia pombe, sigara kwa asilimia 64.4, na shisha kwa asilimia 41.2.

    Unaweza pia kusoma:

  16. Ahadi ya silaha ya Trump inaashiria hatua kubwa kwa Ukraine

    g

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Mkuu wa Nato Mark Rutte alikutana na Trump siku ya Jumatatu

    Kwa mara ya kwanza tangu arejee katika Ikulu ya White House, Donald Trump ameahidi kutoa silaha mpya kwa Ukraine.

    Chini ya mkataba mpya, Marekani itauza silaha kwa wanachama wa Nato ambao watazisambaza kwa Kyiv wakati inapambana na uvamizi wa Urusi.

    Rais hakutoa maelezo mengi kuhusu kile alichosema ni "vifaa vya kijeshi vyenye thamani ya mabilioni ya dola". Lakini alipoulizwa ikiwa mpango huo ulijumuisha betri za ulinzi wa anga za Patriot na makombora ya kupenya, alijibu "ni kila kitu".

    Nchi moja ya Ulaya ina mifumo 17 ya Patriot na "sehemu kubwa" hivi karibuni itakuwa njiani kuelekea Ukraine, Trump alisema.

    Huu ni wakati muhimu.

    Chini ya wiki mbili zilizopita, kulikuwa na hofu katika Kyiv kutokana na habari kwamba Pentagon imesimamisha usafirishaji wa kijeshi kwa Ukraine, ikiwa ni pamoja na Patriots.

    Uamuzi juu ya tangazo hilo bado haujulikani, lakini Jumatatu, Trump alijaribu tena kuliweka hilo wazi , akisema lilifanywa kwa kujua kwamba makubaliano haya yatatimizwa.

    "Tulikuwa na hakika kwamba makubaliano yatafikiwa, kwa hivyo tulisimama kidogo," rais alisema.

    Lakini sasa, kutokana na baadhi ya mazungumzo yataratibu , mengi yakimuhusisha Rutte, silaha zinaweza kuendelea kutiririka bila Washington kuchukua kichupo.

    "Tunatumia pesa nyingi," rais alisema, "na hatutaki kufanya hivyo tena."

    Walipokuwa wamekaa bega kwa bega katika Ofisi ya Oval, Rutte aliendelea kumbembeleza Trump, akiyaita makubaliano ya hivi punde kuwa "makubwa sana" na kusema "ni mantiki kabisa" kwamba wanachama wa Ulaya wa Nato walipie gharama za silaha.

    Unaweza pia kusoma:

  17. Trump atishia kuitoza ushuru Urusi huku akizindua mpango wa silaha wa Ukraine

    h

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Trump

    Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa Marekani itapeleka "silaha za hali ya juu" nchini Ukraine kupitia nchi za Nato, huku pia akitishia kuitoza ushuru Urusi ushuru mkubwa ikiwa makubaliano ya kumaliza vita hayatafikiwa ndani ya siku 50.

    "Tunataka kuhakikisha Ukraine inaweza kufanya kile inachotaka kufanya," Trump alisema kufuatia mkutano na mkuu wa Nato Mark Rutte mjini Washington.

    Rutte alithibitisha kuwa Marekani imeamua "kuipatia Ukraine kwa wingi kile ambacho ni muhimu kupitia Nato" na kwamba Ulaya itazingatia muswada huo.

    Nchi za Ulaya zitaitumia Kyiv mifumo yao ya ulinzi ya anga ya Patriot - ambayo Ukraine inaitegemea kuzuwia mashambulizi mabaya ya anga ya Urusi - na silaha zaidi zitatolewa na Marekani, Trump alisema.

    Si Rutte wala Trump aliyefafanua zaidi kuhusu silaha zitakazotumwa Kyiv lakini Rutte alisema makubaliano hayo yalijumuisha "makombora na risasi".

    Unaweza pia kusoma:

  18. Hujambo na karibu kwa matangaza haya mubashara ya Jumanne 15.07.2025 tukikuletea habari za kikanda na kimataifa