Sudan inawanyanyasa wanawake-HRW

Sudan Kusini inawanyanyasa wanawake -HRW

Chanzo cha picha, Getty

Maelezo ya picha, Sudan Kusini inawanyanyasa wanawake -HRW

Wanaharakati kutoka shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch wamesema kuwa vikosi vya usalama nchini Sudan vinafanya ukatili wa kingono,vitisho na vitendo vingine vinavyokiuka haki za kibinadamu dhidi ya wanawake kwa lengo la kunyamazisha wanaharakati wanawake.

Serikali inawalenga wanaharakati wa kike
Maelezo ya picha, Serikali inawalenga wanaharakati wa kike

HRW linasema kuwa lina takriban mashahidi 12 wa vitendo vya ubakaji vilivyotekelezwa na maafisa wa usalama dhidi ya wanawake wanaopigania haki za kibinadamu.

Aidha HRW linasema kuwa maafisa wao hao wamewatishia wanaharakati wengine na ubakaji.

HRW linasema kuwa lina takriban mashahidi 12 wa vitendo vya ubakaji vilivyotekelezwa na maafisa wa usalama dhidi ya wanawake

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, HRW linasema kuwa lina takriban mashahidi 12 wa vitendo vya ubakaji vilivyotekelezwa na maafisa wa usalama dhidi ya wanawake

Wanaharakati wengine wanasema kuwa maafisa hao wa usalama pia wamewachafulia jina.

HRW inasema kuwa japo ukandamizaji na udhalilishwaji ni jambo la kawaida Sudan , wanawake wanakabiliwa na changamoto ya kipekee.

Maafisa wa serikali nchini Sudan Kusini wamekanusha madai dhidi yao

Chanzo cha picha, Getty

Maelezo ya picha, Maafisa wa serikali nchini Sudan Kusini wamekanusha madai dhidi yao

Maafisa wa serikali nchini Sudan wamekanusha madai ya kudhalilisha wanawake kingono au hata kwa ubakaji.