Coronavirus: Wakenya watekeleza amri ya kutotoka nje usiku kwa siku ya pili

Baadhi ya wakenya wakiamua kutembea kwa mguu kuelekea majumbani mwao ili kuafikia amri ya kutotoka nje usiku iliotolewa na serikali
Maelezo ya picha, Baadhi ya wakenya wakiamua kutembea kwa mguu kuelekea majumbani mwao ili kuafikia amri ya kutotoka nje usiku iliotolewa na serikali
    • Author, Abdalla Seif Dzungu
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Muda wa kusoma: Dakika 2

Amri ya kutotoka nje cnhini Kenya kuanzia 7 moja usiku hadi saa kumi na moja alfajiri imeanza kutekelezwa mwendo wa saa moja huku wafanyakazi wa huduma muhimu pekee wakiruhusiwa kuwa nje usiku.

Hatua hiyo inalenga kuwazuia Wakenya kutangamana katika makundi ya watu nyakati za usiku ili kuzuia kuenea kwa virusi vya ugonjwa wa corona ambavyo tayari vimewaathiri watu 31 huku mtu mmoja akidaiwa kufariki siku ya Alhamisi.

Mwendo wa saa kumi na mbili jioni, Wakenya wengi mjini Nairobi walionekana wakiharakisha kuelekea nyumbani hatua iliosababisha msongamano katika barabara kadhaa huku wale waliokuwa wakitumia magari ya umma wakionekana kusubiri katika vituo vya magari hayo licha ya muda kuyoyoma.

Taarifa zaidi kuhusu coronavirus

Chanzo cha picha, Empics

Wakenya waamua kwenda nyumbani mapema

Matatu chache zilizokuwepo zilitumia fursa hiyo kujitengezea fedha baada ya kuongeza nauli huku baadhi yazo zikikiuka agizo jipya la kupunguza idadi ya abiria ndani ya magari hayo ili kuwaepusha dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona.

Hatahivyo wengine wao walikata kauli na kuanza kutembea kwa miguu wakihofia kukamatwa na maafisa wa polisi.

Inspekta jenerali wa polisi siku ya Ijumaa alionya kwamba wale watakaopatikana nje ya nyumba zao baada ya saa moja usiku watakabiliwa iwezekanavyo.

Mjini Mombasa na Eldoret hatahivyo mpango huo uilianza kwa mkosi baada ya maafisa wa polisi kukabiliana na wakaazi saa mbili kabla ya amri hiyo kuanza kutekelezwa.

Barabara nyingi za mji wa Nairobi zilisalia kuwa mahame mda mfupi kabla ya amri ya kutotoka nje kuanza kutekelezwa
Maelezo ya picha, Barabara nyingi za mji wa Nairobi zilisalia kuwa mahame dakika 30 kabla ya amri ya kutotoka nje kuanza kutekelezwa
Barabara nyingi za mji wa Nairobi zilisalia kuwa mahame dakika 30 kabla ya amri ya kutotoka nje kuanza kutekelezwa
Maelezo ya picha, Barabara nyingi za mji wa Nairobi zilisalia kuwa mahame dakika 30 kabla ya amri ya kutotoka nje kuanza kutekelezwa
Msongamano wa magari huku Wakenya wakiwania kwenda majumbano mwao muda mchache kabla ya amri ya kutotoka nje kutekelezwa
Maelezo ya picha, Msongamano wa magari huku Wakenya wakiwania kwenda majumbano mwao muda mchache kabla ya amri ya kutotoka nje kutekelezwa

Hekaheka kivukoni likoni

Katika mtafaruku huo Maafisa wa polisi waliwachapa mamia ya watumiaji wa kivuko cha likoni ambao walikuwa wamepanga foleni ili kuingia katika kivuko hicho.

Maafoisa hao waliokuwa wamejihami na marungu waliwapiga abiria hao walipojaribu kutumia nguvu kuingia katika kivuko hicho.

Baadhi ya abiria hao walikuwa wakidai kwamba waikuwa wanachalewa kwenda nyumbani mapema ili kuitikia wito wa serikali wa kutumiza amri ya kutotoka nje baada ya saa moja usiku.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Maafisa wa polisi walitumia vitoa machozi kuwatawanya wakaazi hao huku wengine wakiwapiga kwa kutumia marungu.

Wanawake ambao walijipata katika mtafaruku huo walibubujikwa na machozi baada ya kupigwa na kulazimishwa kulala chini na mafisa hao.

Waandishi wa habari pia hawakusazwa huku baadhi yao wakichapwa na polisi kwa kujaribu kurekodi katika kamera zao yaliokuwa yakijiri.

Mkanyangano ulitokea baada ya mamia ya abiria wa kivuko hicho waliokuwa wamekaidi foleni kulazimishwa kurudi katika foleni hizo zilizoanzia katika kania la PCEA karibu na barabara ya Kizingo.

Mjini Eldoret

Wakati huohuo maafisa wa polisi waliwarushia vitoa machozi wakaazi waliokuwa wakiharakisha kwenda nyumbani mjini Eldoret.

Maafisa wa polisi walikuwa wakipiga doria wakiwataka wakaazi kwenda nyumbani.

Wengi wao walirushiwa vitoa machozi bila kujua