Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Salaam za rambirambi zaendelea kutolewa na mashabiki wa Clouds FM baada ya kifo cha Ephraim Kibonde
Salaam za rambirambi zimeendelea kutolewa, baada ya kutokea kifo cha Mfanyakazi na mtangazaji mahiri wa Clouds fm Ephraim Kibonde
Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Dokta Thomas Rutachunzibwa ametoa taarifa kuhusu kifo cha Ephraim Kibonde kilichotokea alfajiri ya siku ya Alhamisi.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Bugando ilipokea mwili wa marehemu Kibonde akitokea hospitali ya Uhuru jijini humo.
Kabla ya kufikishwa Mwanza Kibonde alipata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kagera.
Taarifa ya Mganga mkuu inasema umauti ulimkuta akiwa njiani kuelekea hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya kupata matibabu.
Alianza kujisikia kuumwa tangu alipokua kwenye msiba wa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji marehemu Ruge Mutahaba huko Bukoba.Kisha kupelekwa kwenye hospitali ya Bukoba kabla ya kuamua kumpeleka Mwanza.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga amesema mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam, leo Alhamisi usiku ukitokea jijini Mwanza.
Kibonde alikua mtangazaji mahiri wa kipindi cha JAHAZI cha Clouds fm, kipindi ambacho kimejizolea wasikilizaji wengi kutokana na namna yeye na watangazaji wenzie wanavyowasilisha maudhui mbalimbali ya kipindi hicho kinachoruka majira ya jioni kila siku.