Salaam za rambirambi zaendelea kutolewa na mashabiki wa Clouds FM baada ya kifo cha Ephraim Kibonde

Chanzo cha picha, Mashughuli Blog
Salaam za rambirambi zimeendelea kutolewa, baada ya kutokea kifo cha Mfanyakazi na mtangazaji mahiri wa Clouds fm Ephraim Kibonde
Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Dokta Thomas Rutachunzibwa ametoa taarifa kuhusu kifo cha Ephraim Kibonde kilichotokea alfajiri ya siku ya Alhamisi.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Bugando ilipokea mwili wa marehemu Kibonde akitokea hospitali ya Uhuru jijini humo.
Kabla ya kufikishwa Mwanza Kibonde alipata huduma katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kagera.
Taarifa ya Mganga mkuu inasema umauti ulimkuta akiwa njiani kuelekea hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya kupata matibabu.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 3
Alianza kujisikia kuumwa tangu alipokua kwenye msiba wa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji marehemu Ruge Mutahaba huko Bukoba.Kisha kupelekwa kwenye hospitali ya Bukoba kabla ya kuamua kumpeleka Mwanza.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga amesema mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam, leo Alhamisi usiku ukitokea jijini Mwanza.
Kibonde alikua mtangazaji mahiri wa kipindi cha JAHAZI cha Clouds fm, kipindi ambacho kimejizolea wasikilizaji wengi kutokana na namna yeye na watangazaji wenzie wanavyowasilisha maudhui mbalimbali ya kipindi hicho kinachoruka majira ya jioni kila siku.












