Tetemeko Indonesia: Maeneo yaliyoathirika yafikiwa na huduma ya kwanza, idadi ya waliofariki yaongezeka

Earthquake survivors scuffle to receive food being distributed from a police truck outside a makeshift camp in Palu, Indonesia, on October 2, 2018

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Manusura wakipigana vikumbo kupata chakula cha msaada kutoka kwa lori la polisi nje ya kambi ya muda mjini Palu

Maafisa nchini Indonesia wamesema kuwa wameweza kufikia wilaya zote nne zilizoathiriwa na tetemeko na tsunami mwishoni mwa juma lililopita katika kisiwa cha Sulawesi.

Lakini katika baadhi ya sehemu ni idadi ndogo ya vikosi vya uokoaji vimefika.

Misaada inapelekwa katika sehemu zilizoathiriwa, lakini wanakumbana na changamoto kubwa kutokana na kuharibika kwa miundombinu.

Mpaka sasa zaidi ya watu 1,347 wamethibitishwa kufariki huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka.

Taarifa ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa zaidi ya watu laki mbili walionusurika katika tukio hilo wanahitaji msaada wa haraka.

Palu map
Maelezo ya picha, Ramani ya Palu

Hali hii inajulikana kama Strike-slip, ambayo inaweza kusababisha mawimbi ya hadi urefu wa mita 6 ambayo yaligonga fukwe za mji wa Palu na kumshangaza kila mmoja.

Quake damage

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Tetemeko lilikuwa kubwa lakini sio lile linahusishwa na tukio kubwa la tsunami

Kumbuka kuwa ili kuwepo mawimbi kama hayo ni lazima kuwe na kusonga kwa kiwango kikubwa cha sakafu ya bahari, kitu ambacho kinasababisha maji kusonga kwenda kila upande.

Hesabu za awali zinaonyesha kusonga kwa sakafu ya bahari kwa hadi nusu mita lakini hilo halingeweza kusababisha mawimbi yaliyorekodiwa.

Licha ya kufikia sehemu hizi zilizoathiriwa vibaya, changamoto kubwa inabaki ni namna gani majumba makubwa yaliyoporomoka yanaweza kuondolewa na kupata watu walionasa ndani yake?

Tsunami damage

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Uharibifu za tsunami

Jan Egeland kutoka shirika la wakimbizi nchini Norway na ambaye alikua katika kamati ya maafa ya tsunami ya mwaka 2004 nchini humo ambayo iliua zaidi ya watu laki mbili kutoka eneo la bahari ya Hindi. Anasema kupeleka misaada ya kimataifa sehemu kama hizo ni jambo gumu sana.

Palu city before and after

Chanzo cha picha, PLANET

Maelezo ya picha, Picha za satelaiti zinaonyesha taka ikisombwa upande fulani

Huku haya yote yakiendelea, idadi ya watu waliofariki inatarajiwa kuongezeka na kufikia zaidi ya idadi ya sasa ambayo ni 1350.

Je unajua tsunami zinavyotokea?

Tsunami damage