Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Raila Odinga anafaa kujiita nani kwenye Twitter?
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga alipokuwa kiapo kuwa rais wa wananchi jijini Nairobi Jumanne, mjadala ulizuka kuhusu wadhifa wake.
Alikuwa amekula kiapo kuwa 'Rais wa Kenya' au 'Rais wa Wananchi nchini Kenya'?
Muda haukupita kabla ya utata huo kujitokeza katika maelezo kuhusu ukurasa wake wa Twitter @RailaOdinga.
Awali, ukurasa huo ulikuwa na maelezo kwamba yeye ni kiongozi wa muungano wa upinzani wa National Super Alliance (Nasa).
Muda mfupi baada yake kukamilisha kula kiapo, maelezo yalibadilishwa na akawa 'Rais wa Jamhuri ya Kenya.'
Hapo ndipo utata ulipoanza, kwani Rais Uhuru Kenyatta hujitambulisha pia kama Rais wa Jamhuri ya Kenya.
Muda baadaye, alibadilisha na kuwa kiongozi wa Nasa.
Baadaye usiku, alibadilika na kuwa "Aliyeapishwa kuwa Rais wa Wananchi mnamo 30/1/2018'.
Asubuhi aliondoa maelezo na akabaki tu kuwa 'Mheshimiwa Raila Amolo Odinga'.
Wakenya mtandaoni waligundua hilo:
Sheria za Twitter huharamisha "kujionesha kuwa mtu mwingine kwa njia ya kukanganya au kuhadaa" na ukurasa kama huo unaweza kufungwa kabisa.
"Haufai kujifanya kuwa mtu mwingine, kundi au shirika kwa njia ambayo inanuiwa au inapotosha, kukanganya, au kuwahadaa wengine," zinasema sheria za Twitter.