Raila Odinga anafaa kujiita nani kwenye Twitter?

Chanzo cha picha, AFP/Getty
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga alipokuwa kiapo kuwa rais wa wananchi jijini Nairobi Jumanne, mjadala ulizuka kuhusu wadhifa wake.
Alikuwa amekula kiapo kuwa 'Rais wa Kenya' au 'Rais wa Wananchi nchini Kenya'?
Muda haukupita kabla ya utata huo kujitokeza katika maelezo kuhusu ukurasa wake wa Twitter @RailaOdinga.
Awali, ukurasa huo ulikuwa na maelezo kwamba yeye ni kiongozi wa muungano wa upinzani wa National Super Alliance (Nasa).
Muda mfupi baada yake kukamilisha kula kiapo, maelezo yalibadilishwa na akawa 'Rais wa Jamhuri ya Kenya.'
Hapo ndipo utata ulipoanza, kwani Rais Uhuru Kenyatta hujitambulisha pia kama Rais wa Jamhuri ya Kenya.

Chanzo cha picha, TWITTER
Muda baadaye, alibadilisha na kuwa kiongozi wa Nasa.
Baadaye usiku, alibadilika na kuwa "Aliyeapishwa kuwa Rais wa Wananchi mnamo 30/1/2018'.
Asubuhi aliondoa maelezo na akabaki tu kuwa 'Mheshimiwa Raila Amolo Odinga'.

Chanzo cha picha, TWITTER
Wakenya mtandaoni waligundua hilo:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Sheria za Twitter huharamisha "kujionesha kuwa mtu mwingine kwa njia ya kukanganya au kuhadaa" na ukurasa kama huo unaweza kufungwa kabisa.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
"Haufai kujifanya kuwa mtu mwingine, kundi au shirika kwa njia ambayo inanuiwa au inapotosha, kukanganya, au kuwahadaa wengine," zinasema sheria za Twitter.












