Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ramaphosa aahidi kuimarisha uchumi wa Afrika Kusini
Kiongozi mpya wa chama cha ANC cha Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amefunga rasmi mkutano wa chama hicho akiahidi kufanyia kazi sera za kuimarisha uchumi wa nchi hiyo.
Akizungumza katika kikao kilichomalizika usiku wa manane, Ramaphosa amesema kupambana na rushwa sambamba na umaskini ni kipaumbele cha kwanza kwa chama chake.
Amesema kuwa kikao cha kamati kuu pia kimeahidi kurudisha ardhi muhimu ambazo zilikua mikononi mwa wasiohitajika ikiwa ni lengo la kukuza sekta ya kilimo.
Amemsifu mpinzani wake wa karibu aliyembwaga kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti wa ANC Nkosazana Dlamini Zuma kuwa ni jasiri na mchapa kazi.