Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Video ya kwanza ya wanawake watumwa wa ngono wa Korea yatolewa
Korea Kusini imetoa kile inachokitaja kuwa kanda yake ya kwanza ya wanawake waliolazimishwa kuwa watumwa wa ngono na wanajeshi wa Japan wakati wa vita vya pili va dunia.
Kanda hiyo iliyorekodiwa na wanajeshi wa Marekani nchini China, ilipatwa na wachunguzi waliofadhiliwa na serikali katika chuo cha Seoul kwenye kumbukumbu za Marekani.
Kanda hiyo ya sekunde 18 inaonyesha wanawake kadha wakiwa wamejipanga wakizungumza na mwanajeshi wa China.
Wanaharakati nchini Korea Kusini wanakadiria kuwa wanawake 200,000 walilazimishwa kufanya kazi katika madanguro ya wanajeshi wa Japan.
Wanaaminika kutokea nchini Korea, lakini pia kutoka nchini China, Indonesia , Ufolipino na Taiwan.
Hadi sasa kumbukumbu za wanawake waliolazimishwa kuwa watumwa wa ngono na wanajeshi wa Japan wakti wa vita vya pili vya dunia imekuwani picha na ushuhuda.