Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump ziarani Korea kusini
Rais wa Marekani Donald Trump amewasili Korea ya kusini ikiwa ni sehemu ya ziara yake mashariki mwa Asia.
Katika mtandao wake wa Twitter, Rais Trump amemuelezea Rais wa Korea kusini Moon Jae-in kama mtu mwema na kusema kuwa watafanya kazi pamoja kuweza kushughulikia kitisho cha nyuklia kutoka Korea kaskazini.
Awali Rais Trump alielezea mbinu ya Rais Huyo wa Korea Kusini ambayo ni mbinu shirikishi dhidi ya Korea ya Kaskazini kama ya makubaliano na kwamba raia wa Korea Kusini walikuwa na wasiwasi na kauli za mabavu za Rais Trump kwamba zinaweza kuifanya Korea ya Kaskazini kuchukua hatua za kijeshi katika eneo hilo ya rasi.