Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanamume ampata mamba mkubwa nje ya nyumba yake India
Mwanamume mmoja katika kijiji kilicho jimbo la mashariki mwa India la Orissa, alipigwa na mshangao baada ya kumpata mgeni ambaye hakumtarajia nje ya nyumba yake - mamba wa urefui wa mita 3
Dasharath Madkami alimpata mamba huyo baada ya kuamshwa na sauti zisizo za kawaida usiku.
Alipiga kamsa na wanavijiji wakafika ambao walimfunga mamba huyo kwa mti.
Mamlaka za wanyamapori kisha zikafika kumuokoa mnyama huyo.
Hata hivyo kulikuwa na mzozo kuhusu ni wapi mambaohuyo angepelekwa.
Maafisa wa misitu walitaka kumuachilia myama huyo kwenda kwa bwagwa lililoku karibu ambapo alitoka, lakini wanavijiji wakakataa wakohofia kuwa angerudi tena.
Mamba huyo hata hivyo aliachiliwa kwenda mto Balimela ulio umbali wa kilomita 60.