Dubu amng'ata mgeni kwenye mbuga ya wanyamapori China

Picture of a Chinese visitor to the Badaling Wildlife Park encountering a bear attack

Chanzo cha picha, Weibo/Mr Chen

Maelezo ya picha, Dubu amng'ata mgeni kwenye mbuga ya wanyamapori China

Dubu amemng'ata mgeni kwenye mbuga ya wanyama pori ncjini China sehemu ambayo mwanamke alifarikia dunia baada ya kushambuliwa na dubu mwaka uliopita

Mwanamume huyo alikuwa amepuuza onyo na kuteremsha kioo cha gari lake kuwalisha dubu katika mbuga ya Badaling karibu na mji wa Beijing.

Alinusurika na majeraha madogo.

Tangu wakati huo mamlaka zimeamrisha mbuga hiyo kuboresha hatua za kiusalama ikiwemo kupunguza idadi ya wageni.

Mwaka uliopita mwanamume mmoja na mama yake walitoka ndana ya gari lao ambapo walishambuliwa na duma. Mama alikufa muda baadaye.

Picture of injuries sustained by a Chinese visitor to the Badaling Wildlife Park encountering a bear attack

Chanzo cha picha, Weibo/Mr Chen

Maelezo ya picha, Majeraha ya mng'ato wa Dubu

Katika kisahiki cha siku Ijumaa mwanamme kwa jina Chen, alikuwa akiendesha gari ndani ya mbuga hiyo akiwa na rafiki yake.

Licha ya onyo, wanaume hao waliamua kuteremsha vyoo vya gari lao na kujaribu kuwarushia dubu chakula.

Dubu mmoja alipanda kwenye mlango wa gari na wakati Chen alijaribu kupandisha kio kikakumbwa na hitilabu na badala yake kikaanza kuteremka, ndipo yule dubu akamgata kwenye bega lake.

In a picture taken on 2 June 2010 Chinese visitors sit in their car as they admire lions at the Badaling park near China's Great Wall outside Beijing.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mamlaka za mbuga uruhusu wageni kuendesha magari ndani ya mbuga