Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Dubu amng'ata mgeni kwenye mbuga ya wanyamapori China
Dubu amemng'ata mgeni kwenye mbuga ya wanyama pori ncjini China sehemu ambayo mwanamke alifarikia dunia baada ya kushambuliwa na dubu mwaka uliopita
Mwanamume huyo alikuwa amepuuza onyo na kuteremsha kioo cha gari lake kuwalisha dubu katika mbuga ya Badaling karibu na mji wa Beijing.
Alinusurika na majeraha madogo.
Tangu wakati huo mamlaka zimeamrisha mbuga hiyo kuboresha hatua za kiusalama ikiwemo kupunguza idadi ya wageni.
Mwaka uliopita mwanamume mmoja na mama yake walitoka ndana ya gari lao ambapo walishambuliwa na duma. Mama alikufa muda baadaye.
Katika kisahiki cha siku Ijumaa mwanamme kwa jina Chen, alikuwa akiendesha gari ndani ya mbuga hiyo akiwa na rafiki yake.
Licha ya onyo, wanaume hao waliamua kuteremsha vyoo vya gari lao na kujaribu kuwarushia dubu chakula.
Dubu mmoja alipanda kwenye mlango wa gari na wakati Chen alijaribu kupandisha kio kikakumbwa na hitilabu na badala yake kikaanza kuteremka, ndipo yule dubu akamgata kwenye bega lake.