Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Makamanda wa jeshi wajiuzulu Sudan Kusini
Maafisa watatu wakuu wa kijeshi ndani ya serikali ya Sudan Kusini, wamejiuzulu.
Makamanda hao wamejiondoa serikalini wakimlaumu Rais Salva Kiir kwa kuhusioka katika uhalifu wa kivita na mauwaji yanayolenga kabila fulani.
Brigedia Henry Oyay Nyago, anamshutumu Rais, ambaye anatoka katika kabila la Dinka, kwa kuamuru kuwawa kwa watu wasiotoka katika kabila hilo la Dinka.
Kanali Khalid Ono Loki, pia anamlaumu kiongozi mkuu wa jeshi kwa mauwaji ya kimbari, kukamatwa na kuwazuilia watu kiholela.