Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Sudan Kusini kwenye hatari ya kukumbwa na njaa
Mzozo unaoendelea nchini Sudan Kusini huenda ukachangia kushuhudiwa kwa baa la njaa wakati watu wanaendelea kukimbia makwao na kuacha mazao yao yakioza mashambani, kwa mujibu wa shirika la mpango wa chakula duniani WFP.
Kulingana na WFP hadi watu milioni 4 hawana usalama wa chakula.
Utapiamlo umepita asimia 15 kwenye majimbi Saba kati ya majimbo kumi ambapo majimbo ya Unity na Bahr el Ghazal yameathirika zaidi
Zaidi ya watu milioni moja wameihama nchi hiyo huku watu 4,000 wakivuka na kuingia Uganda kila siku