Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Theluji yaua zaidi ya watu 40 Afghanistan na Pakistan
Theluji nyingi iliyoanguka sehemu za Afghanistan na Pakistan na miporomoko ya barafu, imeuwa watu kadha.
Wakuu wa Afghanistan wanasema watu zaidi ya 40 wamekufa katika majimbo 19, majimbo ya Parwan na Badakhshan ndiyo yameathirika zaidi.
Barabara kuu katika sehemu nyingi za Afghanistan hazipitiki, na uwanja wa ndege mkuu umefungwa.
Theluji nyingi iliyoanguka, imepelekea wakuu kutangaza leo kuwa siku ya likizo.
Na katika nchi jirani ya Pakistan, watu kama 13 wamekufa pale barafu ilipoporomoka na kuzika nyumba kadha.