Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Watu saba wafariki kutokana na dhoruba ya theluji Marekani

Dhoruba hatari ya theluji imeikumba Marekani, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua saba na kukata umeme kwa maelfu ya nyumba.

Muhtasari

Moja kwa moja

Rashid Abdallah

  1. Watu wenye silaha waua watu 11 katika uwanja wa mpira Mexico

    Kundi la washambuliaji wenye silaha limewaua watu 11 na kuwajeruhi 12 katika uwanja wa soka baada ya mechi katika jiji la Salamanca huko Mexico, amesema meya Cesar Prieto, kwenye Facebook siku ya Jumapili.

    Prieto aliongeza kuwa mwanamke na mtoto ni miongoni mwa waliojeruhiwa katika shambulio la "kusikitisha" dhidi ya jamii ya Loma de Flores.

    Uchunguzi umeanzishwa kuhusu shambulio hilo, imesema ofisi ya mwanasheria mkuu katika jimbo la Guanajuato.

    "Wale waliohusika watapatikana," Prieto aliongeza katika maelezo yake ya Facebook.

    Bado haijafahamika sababu ya shambulio hilo lakini Guanajuato ni mojawapo ya majimbo hatari zaidi nchini Mexico.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Watu saba wamefariki kutokana na dhoruba ya theluji Marekani

    Dhoruba hatari ya majira ya baridi imeikumba Marekani, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua saba na kukata umeme kwa maelfu ya nyumba.

    Shule na barabara kote nchini zimefungwa na safari za ndege zimefutwa huku theluti mbaya ikienea kutoka Texas hadi New England, kulingana na Mamlaka ya Kitaifa ya Hali ya Hewa (NWS).

    Watu wawili wamefariki kutokana na baridi kali huko Louisiana, na vifo vingine vinavyohusishwa na dhoruba hiyo vimeripotiwa huko Texas, Tennessee na Kansas.

    Kufikia Jumapili alasiri, zaidi ya kaya 800,000 zimepoteza umeme, kulingana na poweroutage.us. Wakati huo huo, zaidi ya safari za ndege 11,000 zimefutwa, imeripoti FlightAware.

    Theluji nzito inaweza kuathiri takribani Wamarekani milioni 180 - zaidi ya nusu ya idadi ya watu.

    "Theluji na barafu zitayeyuka polepole sana na hazitatoweka hivi karibuni," Allison Santorelli, mtaalamu wa hali ya hewa katika Mamlaka ya Kitaifa ya Hali ya Hewa, ameiambia CBS News.

    Idara ya Afya ya Louisiana imethibitisha Jumapili kwamba wanaume wawili wamefariki kutokana na baridi kali.

    Meya wa Austin, Texas, amesema mtu mmoja amefariki kutokana na baridi.

    Maafisa huko Kansas wamesema mwanamke, ambaye mwili wake ulipatikana Jumapili alasiri ukiwa umefunikwa na theluji, "huenda alikufa kutokana na baridi."

    Vifo vya watu watatu vinavyohusiana na hali ya hewa pia vimeripotiwa huko Tennessee.

    Meya wa Jiji la New York Zohran Mamdani aliandika katika chapisho kwenye X kwamba watu watano katika jiji hilo walifariki Jumamosi lakini akaongeza kuwa chanzo cha vifo vyao bado hakijabainika.

    Marekani inakumbwa na moja ya dhoruba kubwa zaidi za theluji katika zaidi muongo mmoja

    Wataalamu wa hali ya hewa wameonya kwamba moja ya hatari kubwa za dhoruba hiyo ni barafu, ambayo ina uwezo wa kuharibu miti, kuangusha nyaya za umeme na kufanya barabara kuwa hatari.

    Huko Virginia na Kentucky, kumetokea mamia ya ajali barabarani.

    Wacanada pia wamekumbwa na theluji kubwa na mamia ya safari za ndege zilizofutwa.

    Maafisa wanakadiria kwamba kutakuwa na theluji ya sentimita 15-30 (inchi 5-11) katika jimbo la Ontario.

  3. Dhahabu yapanda thamani kutokana na mivutano ya kisiasa na kiuchumi

    Bei ya dhahabu imepanda kwa zaidi ya dola za kimarekani 5,000 (£3,659) kwa gramu 28.35 kwa mara ya kwanza, ni ongezeko la thamani kwa zaidi ya 60% mwaka 2025.

    Hii inakuja huku mvutano kati ya Marekani na NATO kuhusu Greenland ukiongeza wasiwasi kuhusu fedha na siasa.

    Sera za biashara za Rais wa Marekani Donald Trump pia zimetia wasiwasi masoko. Siku ya Jumamosi alitishia kuitoza Canada ushuru wa asilimia 100 ikiwa itaingia makubaliano ya kibiashara na China.

    Dhahabu na madini mengine ya thamani huonekana kama mali salama ambapo wawekezaji hununua wakati wa wasiwasi katika biashara.

    Mahitaji ya madini ya yamechochewa na mambo mengine mbalimbali ikiwa ni pamoja na mfumuko wa bei, dola dhaifu ya Marekani, manunuzi ya benki kuu kote ulimwenguni na huku Hifadhi ya Shirikisho ya Marekani ikitarajiwa kupunguza viwango vya riba tena mwaka huu.

    Vita nchini Ukraine na Gaza, pamoja na Washington kumkamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro, pia vimesaidia kuongeza bei ya dhahabu.

    Pia unaweza kusema:

  4. Watu 15 wafariki baada ya feri kuzama Ufilipino

    Watu wasiopungua 15 wamefariki baada ya feri iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 350 na wafanyakazi wake kuzama kwenye maji ya pwani ya kusini mwa Ufilipino.

    Wafanyakazi wa uokoaji wamewaokoa watu 316 waliokuwa ndani ya meli ya MV Trisha Kerstin 3, lakini watu 28 bado hawajulikani walipo.

    Meli hiyo, ambayo ilikuwa ya mizigo na abiria, ilikuwa njiani kutoka kusini mwa nchi, Mindanao, kwenda kisiwa cha Jolo kusini-magharibi siku ya Jumatatu.

    Serikali inasema wanachunguza chanzo cha kuzama.

    Ufilipino - taifa la visiwa 7,100 - lina historia ndefu ya majanga ya baharini yanayohusisha feri.

    Mei 2023, watu 28 walifariki baada ya kivuko cha abiria kushika moto. Waliofariki ni pamoja na watoto watatu, miongoni mwao mtoto wa miezi sita.

    PIa unaweza kusoma:

  5. Umeme wakatika na vifo vyatangazwa kutokana na dhoruba ya theluji Marekani

    Dhoruba ya theluji imeikumbuka Marekani, na kusababisha vifo vya watu watatu na kukosa umeme kwa maelfu ya nyumba.

    Shule na barabara kote nchini zimefungwa na safari za ndege zimefutwa huku hali "inayohatarisha maisha" ikienea kutoka Texas hadi New England, kulingana na Mamlaka ya Kitaifa ya Hali ya Hewa (NWS).

    Watu wawili wamefariki kutokana na baridi kali huko Louisiana, huku maafisa wa afya wa jimbo wakihusisha vifo vyao na dhoruba hiyo, na kifo kingine kimeripotiwa huko Texas.

    Kufikia Jumapili alasiri, takriban kaya 900,000 zilikuwa zimepoteza umeme, kulingana na poweroutage.us. Wakati huo huo, zaidi ya safari 10,000 za ndege zimefutwa, FlightAware iliripoti.

    "Theluji na barafu zitayeyuka polepole sana na hazitatoweka hivi karibuni," amesema Allison Santorelli, mtaalamu wa hali ya hewa katika Mamlaka ya Kitaifa ya Hali ya Hewa, ameiambia CBS News.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Venezuela yawaachilia huru wafungwa kadhaa wa kisiasa

    Kundi moja la kutetea haki za binadamu nchini Venezuela linasema takribani wafungwa 80 wa kisiasa wameachiliwa huru kutokana na shinikizo la Marekani.

    Alfredo Romero, mkuu wa shirika la Foro Penal, amesema shirika lake linathibitisha utambulisho wa wale walioachiliwa siku ya Jumamosi - na kuna uwezekano wa kuachiliwa wengi zaidi.

    Hilo linatokea tangu Marekani ilipomkamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro, na kumpeleka New York kushtakiwa kwa biashara haramu ya dawa za kulevya mapema mwezi huu.

    Siku ya Ijumaa Rais wa mpito wa Venezuela Delcy Rodriguez alisema zaidi ya wafungwa 600 wameachiliwa huru - lakini Foro Penal inasema takwimu hii imetiwa chumvi.

    Romero alitangaza taarifa hizo kwenye mitandao ya kijamii. Pia alichapisha picha ya mfanyakazi mwenzake wa Foro Penal, Kennedy Tejeda ambaye amesema alishikiliwa katika gereza la Tocorón, magharibi mwa mji mkuu wa Caracas tangu Agosti 2024.

    Makundi ya haki za binadamu na wanaharakati wanaishutumu serikali kwa kuwashikilia wakosoaji. Serikali ya Venezuela imekana kuwashikilia wafungwa wa kisiasa, ikisisitiza kwamba walikamatwa kwa shughuli za uhalifu.

    Wengi walikamatwa baada ya uchaguzi wa rais wa 2024, wakati Maduro alipodai ushindi licha ya upinzani na nchi nyingi kupinga matokeo hayo.

    Pia unaweza kusoma:

  7. Waandamanaji wakusanyika Marekani baada ya afisa wa uhamiaji kutekeleza mauaji

    Umati wa watu umekusanyika Minneapolis, Marekani kupinga uwepo wa maafisa wa uhamiaji wa shirikisho katika jimbo hilo, baada ya kupigwa risasi na kuuawa Alex Pretti mwenye umri wa miaka 37.

    Gavana wa Minnesota Tim Walz ametoa wito kwa Rais wa Marekani, Donald Trump kuwaondoa maafisa hao wa shirikisho katika jimbo lake, akisema: "Huu ni wakati wa mabadiliko."

    Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social, Rais wa Marekani Donald Trump amesema Walz na Meya wa Minneapolis Jacob Frey wanapaswa kuwasalimisha "wahamiaji wote haramu wahalifu" waliofungwa katika magereza ya serikali kwa ajili ya kuwafukuza nchini.

    Maafisa wa jimbo na shirikisho wametoa maelezo yanayokinzana kuhusu tukio la kifo cha Pretti siku ya Jumamosi.

    Alipoulizwa kuhusu video zilizoibuka zikionyesha tukio hilo la mauaji, Kamanda wa Doria ya Mpakani Greg Bovino anasema kuna haja ya kuwepo kwa uchunguzi ili kubaini ukweli.

    Pia unaweza kusoma:

  8. Hujambo na karibu

    Nikukaribishe katika taarifa zetu za moja kwa moja, leo Jumatatu ya tarehe 26, Januari 2026