Moja kwa moja, Waandamanaji wakusanyika Marekani baada ya afisa wa uhamiaji kutekeleza mauaji

Gavana wa Minnesota Tim Walz ametoa wito wake kwa Rais wa Marekani, Donald Trump kuwaondoa maafisa hao wa shirikisho katika jimbo lake, akisema: "Huu ni wakati wa mabadiliko."

Muhtasari

Waandamanaji wakusanyika Marekani baada ya afisa wa uhamiaji kutekeleza mauji

Moja kwa moja

Rashid Abdallah

  1. Venezuela yawaachilia huru wafungwa kadhaa wa kisiasa

    p

    Chanzo cha picha, EPA

    Kundi moja la kutetea haki za binadamu nchini Venezuela linasema takribani wafungwa 80 wa kisiasa wameachiliwa huru kutokana na shinikizo la Marekani.

    Alfredo Romero, mkuu wa shirika la Foro Penal, amesema shirika lake linathibitisha utambulisho wa wale walioachiliwa siku ya Jumamosi - na kuna uwezekano wa kuachiliwa wengi zaidi.

    Hilo linatokea tangu Marekani ilipomkamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro, na kumpeleka New York kushtakiwa kwa biashara haramu ya dawa za kulevya mapema mwezi huu.

    Siku ya Ijumaa Rais wa mpito wa Venezuela Delcy Rodriguez alisema zaidi ya wafungwa 600 wameachiliwa huru - lakini Foro Penal inasema takwimu hii imetiwa chumvi.

    Romero alitangaza taarifa hizo kwenye mitandao ya kijamii. Pia alichapisha picha ya mfanyakazi mwenzake wa Foro Penal, Kennedy Tejeda ambaye amesema alishikiliwa katika gereza la Tocorón, magharibi mwa mji mkuu wa Caracas tangu Agosti 2024.

    Makundi ya haki za binadamu na wanaharakati wanaishutumu serikali kwa kuwashikilia wakosoaji. Serikali ya Venezuela imekana kuwashikilia wafungwa wa kisiasa, ikisisitiza kwamba walikamatwa kwa shughuli za uhalifu.

    Wengi walikamatwa baada ya uchaguzi wa rais wa 2024, wakati Maduro alipodai ushindi licha ya upinzani na nchi nyingi kupinga matokeo hayo.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Waandamanaji wakusanyika Marekani baada ya afisa wa uhamiaji kutekeleza mauaji

    KL

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Umati wa watu umekusanyika Minneapolis, Marekani kupinga uwepo wa maafisa wa uhamiaji wa shirikisho katika jimbo hilo, baada ya kupigwa risasi na kuuawa Alex Pretti mwenye umri wa miaka 37.

    Gavana wa Minnesota Tim Walz ametoa wito kwa Rais wa Marekani, Donald Trump kuwaondoa maafisa hao wa shirikisho katika jimbo lake, akisema: "Huu ni wakati wa mabadiliko."

    Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social, Rais wa Marekani Donald Trump amesema Walz na Meya wa Minneapolis Jacob Frey wanapaswa kuwasalimisha "wahamiaji wote haramu wahalifu" waliofungwa katika magereza ya serikali kwa ajili ya kuwafukuza nchini.

    Maafisa wa jimbo na shirikisho wametoa maelezo yanayokinzana kuhusu tukio la kifo cha Pretti siku ya Jumamosi.

    Alipoulizwa kuhusu video zilizoibuka zikionyesha tukio hilo la mauaji, Kamanda wa Doria ya Mpakani Greg Bovino anasema kuna haja ya kuwepo kwa uchunguzi ili kubaini ukweli.

    Pia unaweza kusoma:

  3. Hujambo na karibu

    Nikukaribishe katika taarifa zetu za moja kwa moja, leo Jumatatu ya tarehe 26, Januari 2026