Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Emmanuel Bushayija atangazwa mfalme mpya wa rwanda
Mwanamume wa miaka 56, mkazi wa Uingereza na ambaye wakati mmoja alifanya kazi katika kampuni ya vinywaji nchini Uganda ametawazwa kuwa mfalme mpya wa Rwanda akiwa uhamishoni.
Mwanamfalme Emmanuel Bushayija amechukua nafasi ya babu yake Mfalme Kigeli V, ambaye alifariki nchini Marekani mwezi Oktoba mwaka jana akiwa na umri wa miaka 80.
Taarifa kutoka kasri ya mfalme zinaarifu kuwa mfalme mpya alilelewa akiwa uhamishoni Uganda na baadaye akafanyia kazi kampuni ya vinywaji ya Pepsi Cola katika mji mkuu wa Kampala.
"Baadaye alijiunga na sekta ya utalii nchini Kenya, kabla ya kurejea Rwanda kati ya mwaka 1994 na 2000. Tangu wakati huo mfalme mpya aliishi Uingereza ambapo alioa na kujaaliwa na watoto wawili," taarifa hiyo imesema.