Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu kadha wafa kwenye ajali ya mashua Tanzania
Watu kadha wanahofiwa kuaga dunia baada ya mashua iliyokuwa safarini kutoka mji wa bandari wa Tanga ikielekea kisiwa cha Pemba kuzama Jumatatu usiku.
Kamanda polisi eneo la kaskazini mashariki, Benedict Wakulyamba, aliiambia BBC kuwa mashua hiyo ilikuwa imewabeba watu 50.
Mkuu huyo wa Polisi alisema kuwa watu tisa wameokolewa na miili 12 kupatikana.
Kilichosababisha kutokea ajali hiyo hakijathibitishwa lakini kamanda wa polisi anasema upepo mkalia huenda ulisababisha mashua hiyo kupoteza mwelekeo.