Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Polisi 29 washtakiwa kwa kutaka kuipindua serikali Uturuki
Takriban maafisa wa polisi 29 wanashtakiwa mjini Instabul Uturuki kwa kuhusika katika jaribio la mapinduzi mnamo mwezi Julai.
Kesi hiyo ndio muhimu zaidi kuwahi kufanyika huku zaidi ya mashtaka 1000 yakiandaliwa. Huku maafisa wengine 40 wakizuiliwa kesi hiyo inatarajiwa kuwa kubwa zaidi katika historia ya Uturuki ya leo.
Washukiwa wanashtakiwa kwa kuwa na lengo la kuipindua serikali mbali na kujihusisha na kundi linaloongozwa na muhubiri anayeishi Marekani Fethullah Gulen, ambaye mamlaka inamlaumu kwa kupanga njama hiyo.