Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Maandamano ya kumpinga Rais yaendelea Korea Kusini
Kwa wiki ya nne mfululizo maelfu ya watu wanaendelea kuandamana katika mji mkuu wa Seoul, nchini Korea Kusini, ili kumshinikiza Rais Park Guen Hye ajiuzulu.
Rais huyo amekataa kuitikia wito wao na kusalia madarakani.
Hapo jana lijitokeza hadharani wa mara ya kwanza, zaidi ya wiki moja, kama ishara ya kuonyesha nia yake ya kutaka kuendelea kuhudumu kama rais.
Waandamanaji hao wameghadhabishwa na hatua yake ya kumruhusu mwanamke anayedaiwa kuwa rafiki yake wa karibu, Choi Soon-sil, kutumia ushawishi wake kufanya ulaghai.
Mwanamke huyo kwa sasa anazuiliwa na maafisa wa usalama.