Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Morsi aondolewa hukumu ya kifo
Mahakama nchini Misri imebatilisha hukumu ya kifo aliyopewa rais aliyepinduliwa Mohammed Morsi.
Morsi alikumiwa kifo baada ya kulaumiwa kuhusika na kutoroka kwa wafungwa wengi wakati wa mapinduzi ya mwaka 2011.
Alichaguliwa kuwa rais mwaka 2012 lakini akaondolewa na jeshi mwaka mmoja baadaye, kufuatia maandamano makubwa ya kupinga utawala wake.
Morsi ashahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa mashtaka yanayohusu ugaidi na bado anakabiliwa na mashtaka kwa makosa mengine.