Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kenyatta: Tuna haki kuondoa majeshi Sudan Kusini
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametetea hatua ya nchi yake na kuwaondoa wanajeshi wake kutoka kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini Sudan Kusini.
Rais Kenyatta alisema kuwa Kenya imejitolea katika kuchangia amani katika kanda hii na dunia nzima lakini akaongeza kuwa heshima ya nchi haiwezi kuchafuliwa.
Bwana Kenyatta alikuwa akizungumza wakati aliongoza hafla ya kufuzu kwa wanajeshi kwenye chuo cha kutoa mafunzo ya kijeshi cha Lanet kaunti ya Nakuru.
Alisema kuwa uamuzi wa kuondoka kwenye mpango huo wa amani, unafuatia visa vinavyaokua ujumbe wa umoja wa mataifa nchini Sudan Kusini, ambapo Umoja wa Mataifa ulimlaumu kamada kutoka nchini Kenya.
Kenyatta aliongeza pia kuwa Kenya ina mpamgo ya kuwaondoa wanajeshi wake kutoka ujumbe huo ambao alisema umeanza kuwalaumu wakenya.
Kenyatta alisema kuwa kenya imachangia makanda wenye tajriba ya juu katika masuala ya kulinda amani wakiwemo Luteni Jenerali Daniel Opande ambaye alikuwa kamanda wa kikosi cha kulinda amanai nchini Sierra Leone na Luteni Jenerali Ngondi ambaye alikuwa kamanda nchini Liberia miongoni mwa wengine.