Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ban Ki-moon akosoa pendekezo la Netanyahu kuhusu upanuzi wa makazi ya Israel
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon amemkosoa vikali waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwa pendekezo lake kwa wale wanaopinga upanuzi wa makazi ya Israel kuwa wao ni wafuasi wa kikabila.
Ban Ki-moon amesema kuwa maoni ya Netanyahu hayakubaliki na ni ya kichochezi.
Ban Ki-moon ambae anaondoka madarakani mwisho wa mwaka huu amewakumbusha Israel kuwa upanuzi huo wa makazi sio halali chini ya sheria ya kimataifa, na kwa lugha ya ukali Ban Ki-moon alisema Urusi lazima imalize ukandamizaji na uvamizi wa maeneo ya Palestina.