Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kofi Annan aonywa asiingilie masuala ya Myanmar
Mamia ya wanaharakati wa Kibudha nchini Myanmar wamemzomea katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, alipowasili katika jimbo la Rakhine.
Bw Annan aliombwa na kiongozi wa Myanmar, Aung San Suu Kyi, kuongoza tume itakayochunguza mzozo wa kijamii katika jimbo hilo lililoko magharibi mwa nchi.
Wanaompinga wanasema suala hilo ni suala la ndani ya nchi na kwamba wageni hawapasi kuingilia masuala yao.
Maelfu kwa maelfu ya jamii ya dhehebu la Waislam wa Rohingya wamesambaratika kutokana na mashambulio ya mabudha walio wengi. Wengi wamekimbia nchi.
Ghasia hizo zimesababisha baadhi kuhoji juhudi za Aung San Suu Kyi za haki za kibinadamu nchini hum