Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mafuriko yasababisha vifo kaskazini mwa India
Mafuriko makubwa yaliyokumba eneo la kaskazini na kati ya India yamesababisha vifo vya zaidi ya watu mia moja hamsini.
Kwa mujibu wa serikali watu wengine milioni mbili nukta nne wameathiriwa katika jimbo la Bihar na miji mingine ya mashariki huku viwango vya maji katika mto Ganges vikizidi kuongezeka.
Maelfu ya watu wamepewa hifadi katika kambi lakini wengine hawataki kuondoka majumbani mwao.
Shirika la misaada la ActionAid limesema kumekuwa na uharibifu mkubwa hasa katika mashamba ya mpunga ambao huenda kukasababisha upungufu wa chakula.