Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
"Kuna watu wanasema natumia dawa, wananiita mchawi, lakini si kweli" -Mtaalamu wa kushika nyuki
Kutana na kijana Athuman Masimba aka Masimba Nyuki ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kwa kuyahamisha makundi ya nyuki kwa kutumia mikono bila ya nyuki hao kumdhuru.
Athuman amekua akienda sehemu mbalimbali kwa lengo la kusaidia kuhamisha nyuki ambao wangeweza kuleta madhara kwa watu
Baadhi wanaona anatumia nguvu za giza kufanya hivyo, ila yeye anasema ni mapenzi yake kwa wadudu hao ndio yanamfanya wasimdhuru.
Mwandishi wa BBC @mcdavid_nkya_ alikutana nae Mkoani Geita Kaskazini Magharibi mwa Tanzania.