Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wasira: Martha Karua kawaponza wanaharakati wengine
Chama tawala nchini Tanzania CCM kimesema suala la mwanasiasa wa Kenya Martha Karua kuingilia maamuzi ya mahakama ya nchi hiyo ndio lililosababisha kuzuiliwa kwa wanaharakati wengine waliotaka kuja kushuhudia kesi ya mwanasiasa wa upinzani Tundu Lissu.
Katika mahojiano maalum na BBC, Makamu mwenyekiti wa chama hicho, Stephen Wasira amesema hatua hiyo ilikua ni kama kuingilia maamuzi ya ndani ya nchi kitu ambacho hakikubaliki.
Ameanza kwa kumuelezea mwandishi wa BBC David Nkya malalamiko ya kwamba vyombo vya dola nchini humo vinatumika kuukandamiza upinzani.