Vifaa vya microchips: Rasilimali ya thamani inayopiganiwa na nchi za Marekani na China

Kwa zaidi ya karne moja kupigania mafuta kulizua vita, kulazimisha miungano isiyotarajiwa na kuzua migogoro mingi ya kidiplomasia.

Sasa mataifa makubwa zaidi ya kiuchumi duniani yanapigania rasilimali nyingine ya thamani: vifaa vya microchips ambavyo ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku

Vifaa hivi vidogo vya silicon ndio kiini cha sekta ya dola bilioni 500, inayotarajiwa kuongezeka maradufu ifikapo mwaka 2030. Na yeyote anayedhibiti mifumo ya usambazaji - mtandao wa kampuni na nchi zinazotengeneza microchips - anamiliki ufunguo wa kuwa nguvu kuu.

China inataka teknolojia hiyo kuzalisha microchips, ndiyo maana Marekani, chimbuko la teknolojia nyingi, inaitenga Beijing.

Nchi hizo mbili ziko wazi katika mashindano ya silaha katika eneo la Asia Pacific, anasema Chris Miller, mwandishi wa Chip Wars na profesa msaidizi katika Chuo Kikuu cha Tufts huko Massachusetts, Marekani.

Na anaongeza kuwa kuna mambo zaidi katika mbio hizo.

"Inafanyika katika nyanja kama vile idadi ya meli au makombora yanayotengenezwa, lakini pia hufanyika katika suala la ubora wa akili za bandia (AI) ambazo zinaweza kutumiwa katika mifumo ya kijeshi." .

Kwa sasa, Marekani inashinda, lakini vita vya microchip vilivyotangazwa dhidi ya China vinarekebisha uchumi wa dunia.

Watengezaji

Utengenezaji wa microchips ni mfumo mgumu, maalumu, na umeunganishwa kwa kina

Simu ya IPhone ina microchips ambazo zimeundwa nchini Marekani, zinazozalishwa Taiwan, Japan au Korea Kusini, na kisha kuunganishwa nchini China. India, ambayo inawekeza sana katika sekta hii, inaweza kuchukua jukumu muhimu katika siku zijazo.

Microchips zilivumbuliwa nchini Marekani, lakini baada ya muda Asia Mashariki imekuwa kituo chao cha uzalishaji, hasa kwa sababu ya motisha na ruzuku ya serikali.

Hii imeruhusu Washington kukuza uhusiano wa kibiashara na ushirikiano muhimu katika eneo ambalo linaweza kuathiriwa na Urusi wakati wa Vita Baridi. Na hizi bado ni muhimu sana leo katika ushawishi unaozidi sasa wa Uchina katika eneo la Asia-Pasifiki.

Nanomita

Shindano linahusu kutengeneza microchip bora na kwa wingi, na ndogo zaidi. Ni changamoto ya transistors ngapi, swichi ndogo za umeme zinazoweza kuzima au kuruhusu mkondo kupita, kutoshea kwenye kipande kidogo zaidi cha silikoni.

"Ni kile ambacho sekta ya semiconductor inaita sheria ya Moore, ambayo kimsingi inaongeza mara dufu msongamano wa transistors kwa muda, na hilo ni lengo gumu sana kufikiwa," anasema Jue Wang, mshirika katika kampuni ya ushauri ya Bain & Company huko Silicon Valley, California.

"Hilo ndilo linalofanya simu zetu ziwe na kasi zaidi, kumbukumbu zetu za picha za kidijitali kuwa kubwa, vifaa vyetu kuwa nadhifu kadri muda unavyopita, na maudhui yetu ya mitandao ya kijamii kuwa bora zaidi."

Kufikia hilo si rahisi hata kwa wazalishaji wakuu wa microchips.

Katikati ya mwaka 2022, Samsung ilifanikiwa kuwa kampuni ya kwanza kuanza uzalishaji wa wingi wa microchips za kiwango cha nanomita tatu.

Jambo ambalo Kampuni ya Kutengeneza microchip ya Taiwan (TSMC), mtengenezaji mkubwa zaidi wa microchip duniani na msambazaji kwa Apple, pia iliweza kufanya mwishoni mwa mwaka huo.

Ili kukupa wazo, tunazungumza juu ya mistari laini zaidi kuliko nywele ya binadamu, ambayo ni kati ya nanomita 50 na 100,000.

Vifaa hivi vidogo pia vina nguvu zaidi, ambayo ina maana kwamba vimejumuishwa katika vifaa vya thamani zaidi kama vile kompyuta kuu na bidhaa za akili bandia.

Microchips nyingi za ulimwengu zinatengenezwa nchini Taiwan, na kukipa kisiwa hicho kidogo kile rais wake anachokiita "ngao ya silicon," ambayo kwa maneno mengine inamaanisha ulinzi kutoka kwa Uchina, ambayo inaendelea kudai eneo hilo kama lake.

Beijing pia imefanya uzalishaji wa microchip kuwa kipaumbele cha kitaifa na inawekeza kwa nguvu katika kompyuta kubwa na akili bandia. Bado hakuna mahali karibu na kuwa mmoja wa viongozi wa ulimwengu katika eneo hili, lakini katika miaka kumi iliyopita imekuja karibu sana, juu ya yote, Profesa Miller anasema, katika uwezo wake wa kubuni microchips.

"Unachokipata kihistoria ni kwamba kila wakati nchi zenye nguvu zaidi zinapopiga hatua katika teknolojia, wanachofanya ni kutekeleza katika mifumo yao ya kijasusi na kijeshi," aliongeza.

Ni hili, na tegemeo lake kwa Taiwan na nchi nyingine za Asia kukidhi mahitaji yake, ambayo inasumbua Marekani.

Je, Marekani inaizuia vipi China?

Utawala wa Biden unajaribu kuzuia ufikiaji wa China kwa teknolojia ya microchip.

Mnamo Oktoba mwaka jana, Washington ilitangaza mfululizo mkubwa wa udhibiti ambao unafanya iwe vigumu kwa makampuni kusafirisha microchips, mashine zinazozitengeneza, au programu zenye teknolojia ya Marekani kwa China bila kujali ziko wapi duniani.

Pia ilipiga marufuku raia wake au wakazi wa nchi yake kusaidia "maendeleo au uzalishaji" wa microchips katika viwanda fulani nchini China.

Hili limegusa gwiji huyo wa Asia, ambaye anategemea vipaji vya watu ili kuchochea sekta yake changa ya kutengeneza chips.

 “Vipaji ni muhimu sana katika sekta hii, ukiangalia wakuu wa makampuni ya Kichina ya kutengeneza microchips wengi wao wana pasi za kusafiria za Marekani, wamesoma au wameendelezwa nchini humo na wana green card, hilo ni tatizo kubwa kwa China,” alisema Linghao Bao mchambuzi wa utafiti wa sera katika Trivium China.

Marekani, kwa upande wake, pia inataka kuzalisha microchips zaidi. Kwa mujibu wa sheria ya CHIPS na Sayansi, baadhi ya Dola za Marekani milioni 53,000 hutolewa kama ruzuku kwa makampuni ambayo yanaamua kutengeneza microchips nchini Marekani.

Hii ni faida kwa makampuni makubwa kama TSMC, ambayo inawekeza katika mitambo miwili yenye thamani ya dola bilioni 40 za Marekani, ambayo ni ya kwanza nje ya Taiwan.

Micron, mtengenezaji mkuu zaidi wa microchips za kumbukumbu nchini Marekani muhimu kwa kompyuta kubwa, vifaa vya kijeshi na kifaa chochote kinachojumuisha kichakataji, ilitangaza mipango ya kuwekeza takriban dola bilioni 100 katika kipindi cha miaka 20 ijayo katika kiwanda cha kutengeneza microchips nchini Marekani jimbo la New York.

"Sheria inaturuhusu kupunguza tofauti za gharama za uzalishaji zilizopo Marekani dhidi ya zile za Asia," alisema Sanjay Mehrotra, Mkurugenzi Mtendaji wa Micron Technology.

"Micron itaendelea kuwekeza kwenye mitambo yetu barani Asia. Cha muhimu ni kwamba kutakuwa na usawa katika sekta hiyo duniani kote."

Jukumu la China

Vizuizi vya Amerika vinaumiza Uchina ambapo inaumiza sana.

Kuna taarifa kwamba Apple imeachana na mpango wa kununua microchips za kumbukumbu kutoka kwa kampuni moja iliyofanikiwa zaidi nchini China, Yangtze Memory Technologies Corp (YMTC) kutokana na vikwazo hivyo.

Na kilichotokea dhdi Huawei huenda ukarudiwa tena, Bao anaonya.

Kampuni hiyo kubwa ya mawasiliano ilitoka kuwa mtengenezaji wa pili kwa ukubwa wa kutengeneza simu duniani nyuma ya Samsung hadi karibu kufa.

"Ilikuwa rahisi kwa Washington kuangusha kampuni ya teknolojia ya Kichina na Beijing haina chaguo wazi kujibu mpango huo," Bao aliongeza.

"Hapo awali, Marekani ililenga makampuni binafsi, lakini wakati huu shughuli zake zimeenea hadi nchi nzima."

Kwa hivyo kuna chochote China inaweza kufanya? Kutoa bidhaa na huduma zako au kuweka vidhibiti vyako vya kusafirisha nje kunaweza kukudhuru zaidi kuliko manufaa, hasa wakati uchumi wako unadorora sana.

Beijing ililalamika kwa Shirika la Biashara Duniani (WTO), lakini azimio kutoka kwa chombo hicho linaweza kuchukua miaka.

Wakati huo huo, wataalam wanasema, China inaweza kupunguza maradufu katika uwekezaji ili kusaidia sekta yake ya microchip.

"Tutazingatia mahitaji ya kimkakati ya kitaifa, kukusanya nguvu zetu kufanya utafiti wetu wa kisayansi na kiteknolojia kwa dhamira ya kushinda vita katika sekta muhimu za teknolojia," Rais Xi Jinping alisema kwenye kongamano la Chama cha Kikomunisti mnamo Oktoba mwaka jana.

Nini kinafuata?

Kwa muda mfupi, sekta inakabiliwa na mzozo wa kiuchumi unaotokana na vita nchini Ukraine, mfumuko wa bei wa juu na kufunguliwa tena kwa uchumi wa China.

Kwa sababu ya athari za janga la corona, China hakika itasonga kwa uangalifu sana.

"Kutakuwa na mvutano mwingi kati ya makampuni ya Marekani, makampuni ya Taiwan, makampuni ya Kichina na kila kampuni nyingine kutoka nchi ingine. Itakuwa tu ambapo microchips za kumbukumbu za juu zinahitajika kwamba tutaona jitihada za kweli kutoka Washington kutenga Uchina kutoka kwa mitandao ya uvumbuzi na juhudi za Beijing kujenga mkondo wake wa usambazaji bila uwepo wa Marekani," Miller alihitimisha.

Hiyo, anaongeza, inaweza kumaanisha kutengana kwa mfumo wa ikolojia, moja iliyojilimbikizia Uchina na nyingine katika ulimwengu wote.

Hii itakuwa na athari kwa uchumi wa dunia na italazimisha pande zote kuchagua upande, na hatari inayowezekana kwamba wengi hawataweza kufikia soko la China.